Mwanzo › Sura › Sura Ash-Shu'araa
Sura Ash-Shu'araa الشعراء
Aya 227 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 47
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ طسٓمٓ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tw'a Siin Miim.[1]
Tazama tafsiri zote za aya hii →
تِلْكَ ءَايَٰتُ ٱلْكِتَٰبِ ٱلْمُبِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَعَلَّكَ بَٰخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةً فَظَلَّتْ أَعْنَٰقُهُمْ لَهَا خَٰضِعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ ٱلرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهُ مُعْرِضِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَقَدْ كَذَّبُوا۟ فَسَيَأْتِيهِمْ أَنۢبَٰٓؤُا۟ مَا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa yakini wamekwishakanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوَلَمْ يَرَوْا۟ إِلَى ٱلْأَرْضِ كَمْ أَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئْتِ ٱلْقَوْمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَوْمَ فِرْعَوْنَ أَلَا يَتَّقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبِّ إِنِّىٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَيَضِيقُ صَدْرِى وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِى فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَٰرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَهُمْ عَلَىَّ ذَنۢبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ كَلَّا فَٱذْهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ ٱلَّتِى فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلْكَٰفِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ فَعَلْتُهَآ إِذًا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipokuwa miongoni mwa wale waliopotea.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِى رَبِّى حُكْمًا وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi nikawakimbia nilipowahofu, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَىَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hiyo ndiyo neema ya kunisimbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Firauni akasema: Na ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُۥٓ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Firauni) akawaambia waliomzunguka: Kwani hamsikilizi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِىٓ أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliyetumwa kwenu ni mwendawazimu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَآ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِى لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ ٱلْمَسْجُونِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Firauni) akasema: Ukijifanyia mungu mwingine asiyekuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَىْءٍ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Je, hata kama nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ فَأْتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wakweli.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِىَ بَيْضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na akautoa nje mkono wake, mara ukawa mweupe kwa watazamao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Firauni) akawaambia waheshimiwa waliomzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِۦ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Anataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَٱبْعَثْ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Mpe muda yeye na kakaye na uwatume mijini wakusanyao watu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يَأْتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wakakusanywa wachawi kwa ajili ya miadi ya siku maalumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَٰلِبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Huenda tutawafuata wachawi ikiwa wao ndio watakaoshinda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُوا۟ لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ ٱلْغَٰلِبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi walipokuja wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa sisi ndio tutakaoshinda?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ ٱلْمُقَرَّبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Ndiyo! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلْقُوا۟ مَآ أَنتُم مُّلْقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Musa akawaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَلْقَوْا۟ حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا۟ بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ ٱلْغَٰلِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِىَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza vile walivyovizua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hapo wachawi hao walipinduka wakasujudu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mola Mlezi wa Musa na Harun.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَٰفٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Firauni) akasema: Je, mmemuamini kabla ya kuwaruhusu? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliyewafunza uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitawasulubisha misalabani nyote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ لَا ضَيْرَ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika sisi tunatumai kwamba Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa tumekuwa wa kwanza wa Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِىٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tulimuamrisha Musa kwa ufunuo: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِى ٱلْمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi Firauni akawatuma mijini wakusanyaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَآئِظُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Nao kwa hakika wanatuudhi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَخْرَجْنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi tukawatoa katika mabustani na chemchemi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mahazina, na vyeo vya heshima,
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَٰهَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Vivyo hivyo, na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wakawafuata lilipochomoza jua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumekutwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ كَلَّآ إِنَّ مَعِىَ رَبِّى سَيَهْدِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضْرِب بِّعَصَاكَ ٱلْبَحْرَ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَٱلطَّوْدِ ٱلْعَظِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tulimletea Musa ufunuo tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ ٱلْـَٔاخَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawasongesha hapo karibu wale wengine.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tukawaokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha tukawazamisha hao wengine.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَٰهِيمَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wasomee habari za Ibrahim.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَا تَعْبُدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Je, yanawasikia mnapoyaita?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Au yanawafaa, au yanawadhuru?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ بَلْ وَجَدْنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Bali tuliwakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ أَفَرَءَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: "Je, mmewaona hawa mnaowaabudu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلْأَقْدَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Nyinyi na baba zenu wa zamani?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّىٓ إِلَّا رَبَّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلَّذِى خَلَقَنِى فَهُوَ يَهْدِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلَّذِى هُوَ يُطْعِمُنِى وَيَسْقِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ninapougua, ni Yeye ndiye anayeniponesha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلَّذِى يُمِيتُنِى ثُمَّ يُحْيِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلَّذِىٓ أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِى خَطِيٓـَٔتِى يَوْمَ ٱلدِّينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ambaye ndiye ninayemtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
رَبِّ هَبْ لِى حُكْمًا وَأَلْحِقْنِى بِٱلصَّٰلِحِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na walio wema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱجْعَل لِّى لِسَانَ صِدْقٍ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na unijalie nitajwe kwa wema na watu watakaokuja baadaye.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱجْعَلْنِى مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na unijalie katika warithi wa Bustani za neema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱغْفِرْ لِأَبِىٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَا تُخْزِنِى يَوْمَ يُبْعَثُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala usinihizi Siku watakapofufuliwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Siku ambayo kwamba mali haitafaa kitu wala wana.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا مَنْ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأُزْلِفَتِ ٱلْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Bustani ya mbiguni itasogezwa kwa wacha Mungu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَبُرِّزَتِ ٱلْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wataambiwa: Wako wapi mliokuwa mkiwaabudu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, wanawasaidia, au wanajisaidia wenyewe?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكُبْكِبُوا۟ فِيهَا هُمْ وَٱلْغَاوُۥنَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na majeshi ya Ibilisi yote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
Tazama tafsiri zote za aya hii →
تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِى ضَلَٰلٍ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center "Tallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tulipowafanya nyinyi ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلْمُجْرِمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hawakutupoteza isipokuwa wale wakosefu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hatuna waombezi wowote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala rafiki wa dhati.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Laiti tungelipata kurejea tena, tungelikuwa katika Waumini."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je, hamumchi Mwenyezi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na siwaulizi juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ أَنُؤْمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلْأَرْذَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Je, tukuamini wewe, ilhali wanaokufuata ni watu duni?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ وَمَا عِلْمِى بِمَا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Ninayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّى لَوْ تَشْعُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Mola wao Mlezi, laiti mngelitambua!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنْ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mimi si chochote isipokuwa ni Mwonyaji wa dhahiri shahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمَرْجُومِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِى كَذَّبُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱفْتَحْ بَيْنِى وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِى وَمَن مَّعِىَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَنجَيْنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa hivyo tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika marikebu iliyosheheni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ ٱلْبَاقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha tukawazamisha baadaye waliobakia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao waliokuwa Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ عَادٌ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kina 'Aad waliwakanusha Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipowaambia ndugu yao, Hud: Je, hamumchi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala siwaulizi juu yake ujira wowote, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةً تَعْبَثُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mnajenga majengo ya kifahari kama kwamba mtaishi milele!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mnapotumia nguvu, mnatumia nguvu kwa ujabari.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِىٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mcheni aliyewapa haya mnayoyajua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَمَدَّكُم بِأَنْعَٰمٍ وَبَنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Aliwapa wanyama wa kufuga na wana.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mabustani na chemchemi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّىٓ أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika mimi ninawahofia adhabu ya Siku Kubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْنَآ أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ ٱلْوَٰعِظِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنْ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Haya si chochote isipokuwa ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala sisi hatutaadhibiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَٰهُمْ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakamkadhibisha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ ثَمُودُ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kina Thamud waliwakadhibisha Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipowaambia ndugu yao Saleh: Je, hamumchi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَتُتْرَكُونَ فِى مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, mtaachwa salama salimini katika haya yaliyopo hapa?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فِى جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Katika mabustani, na chemchemi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na konde na mitende yenye makole yaliyowiva.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًا فَٰرِهِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَا تُطِيعُوٓا۟ أَمْرَ ٱلْمُسْرِفِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala msitii amri za waliopitiliza mipaka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ambao wanafanya uharibifu katika nchi, wala hawatengenezi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wewe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi. Basi leta Ishara ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala msimguse kwa wovu, ikawashika adhabu ya Siku Kubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا۟ نَٰدِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Lakini wakamuua, na wakawa wenye kujuta.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَخَذَهُمُ ٱلْعَذَابُ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watu wa Luti waliwakadhibisha Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipowaambia ndugu yao, Luti: Je, hamumchi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala mimi sikuwauliza ujira wowote juu yake; ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَتَأْتُونَ ٱلذُّكْرَانَ مِنَ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَٰجِكُم بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mnaacha alichowaumbia Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلْمُخْرَجِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Ewe Luti! Usipoacha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa mji!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ إِنِّى لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلْقَالِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
رَبِّ نَجِّنِى وَأَهْلِى مِمَّا يَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَنَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَٰبِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha tukawaangamiza wale wengine.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا فَسَآءَ مَطَرُ ٱلْمُنذَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyoonywa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَ أَصْحَٰبُ لْـَٔيْكَةِ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Shuaibu alipowaambia: Je, hamumchi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِىَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوْفُوا۟ ٱلْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا۟ مِنَ ٱلْمُخْسِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Timizeni kipimo sawasawa, wala msiwe katika wanaopunja.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَزِنُوا۟ بِٱلْقِسْطَاسِ ٱلْمُسْتَقِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na pimeni kwa haki iliyonyooka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَا تَبْخَسُوا۟ ٱلنَّاسَ أَشْيَآءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا۟ فِى ٱلْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri katika ardhi kwa kufanya uharibifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱتَّقُوا۟ ٱلَّذِى خَلَقَكُمْ وَٱلْجِبِلَّةَ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلْمُسَحَّرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Hakika wewe ni katika waliorogwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلْكَٰذِبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wewe si chochote isipokuwa ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبِّىٓ أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayoyatenda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ ٱلظُّلَّةِ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya Siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya Siku kubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلْأَمِينُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ameuteremsha Roho muaminifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلْمُنذِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بِلِسَانٍ عَرَبِىٍّ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّهُۥ لَفِى زُبُرِ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ ءَايَةً أَن يَعْلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُا۟ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanachuoni wa Wana wa Israili?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَوْ نَزَّلْنَٰهُ عَلَىٰ بَعْضِ ٱلْأَعْجَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na lau kuwa tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَقَرَأَهُۥ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا۟ بِهِۦ مُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَٰلِكَ سَلَكْنَٰهُ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wahalifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُا۟ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana habari.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَيَقُولُوا۟ هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na watasema: "Je, tutapewa muhula?"
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi je, wanaihimiza adhabu yetu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَفَرَءَيْتَ إِن مَّتَّعْنَٰهُمْ سِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُوا۟ يُوعَدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha yakawafikia waliyokuwa wakiahidiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يُمَتَّعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Yatawafaa nini yale waliyostareheshewa?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala Mashetani hawakuteremka nayo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا يَنۢبَغِى لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُمْ عَنِ ٱلسَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika hao wametengwa na kusikia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَا تَدْعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلْمُعَذَّبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ ٱلْأَقْرَبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na watwae kwa upole wanaokufuata miongoni mwa Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّى بَرِىٓءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ikiwa watakuasi, basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyatenda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَوَكَّلْ عَلَى ٱلْعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلَّذِى يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ambaye anakuona unaposimama.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَقَلُّبَكَ فِى ٱلسَّٰجِدِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mageuko yako katika wanaosujudu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua zaidi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, niwaambieni nani wanawashukia Mashetani?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يُلْقُونَ ٱلسَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَٰذِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wanawapelekea yale wanayoyasikia; na wengi wao ni waongo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلْغَاوُۥنَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na watungaji mashairi ni wapotovu ndio wanawafuata.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِى كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwamba wao husema wasiyoyatenda?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُوا۟ ٱللَّهَ كَثِيرًا وَٱنتَصَرُوا۟ مِنۢ بَعْدِ مَا ظُلِمُوا۟ وَسَيَعْلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓا۟ أَىَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na wanaodhulumu watakuja jua mgeuko gani watakaogeuka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
← Sura Al-Furqaan
Sura An-Naml →
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
→
Matini ya Kiarabu na tafsiri kupitia Tanzil na QuranEnc — kama zilivyo, bila kubadilishwa · Tafsiri ni mali ya watafsiri wake na si Qur'ani yenyewe
Hii ni nyenzo ya utafiti, si chanzo cha fatwa.