caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Al-Furqaan الفرقان

Aya 77 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 42

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ تَبَارَكَ ٱلَّذِى نَزَّلَ ٱلْفُرْقَانَ عَلَىٰ عَبْدِهِۦ لِيَكُونَ لِلْعَٰلَمِينَ نَذِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmetukuka aliyeteremsha Furqani kwa mja wake, ili awe mwonyaji kwa walimwengu wote.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَلَمْ يَتَّخِذْ وَلَدًا وَلَمْ يَكُن لَّهُۥ شَرِيكٌ فِى ٱلْمُلْكِ وَخَلَقَ كُلَّ شَىْءٍ فَقَدَّرَهُۥ تَقْدِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbaye ni wake ufalme wa mbingu na ardhi, wala hakuwa na mwana, wala hakuwa na mshirika katika ufalme, na akaumba kila kitu na akakikadiria kwa kipimo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱتَّخَذُوا۟ مِن دُونِهِۦٓ ءَالِهَةً لَّا يَخْلُقُونَ شَيْـًٔا وَهُمْ يُخْلَقُونَ وَلَا يَمْلِكُونَ لِأَنفُسِهِمْ ضَرًّا وَلَا نَفْعًا وَلَا يَمْلِكُونَ مَوْتًا وَلَا حَيَوٰةً وَلَا نُشُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wamechukua badala yake miungu ambayo haiumbi chochote, bali hiyo inaumbwa, haijimilikii nafsi zao madhara wala manufaa, wala haimiliki mauti, wala uhai, wala kufufuka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓا۟ إِنْ هَٰذَآ إِلَّآ إِفْكٌ ٱفْتَرَىٰهُ وَأَعَانَهُۥ عَلَيْهِ قَوْمٌ ءَاخَرُونَ فَقَدْ جَآءُو ظُلْمًا وَزُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wamesema waliokufuru: "Haya si chochote ila ni uzushi aliouzua, na wamemsaidia kwa haya watu wengine!" Hakika hawa wamekuja na dhuluma na uongo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالُوٓا۟ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ ٱكْتَتَبَهَا فَهِىَ تُمْلَىٰ عَلَيْهِ بُكْرَةً وَأَصِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wakasema: Hivi ni visa vya watu wa kale alivyoviandikisha, anavyosomewa asubuhi na jioni.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُلْ أَنزَلَهُ ٱلَّذِى يَعْلَمُ ٱلسِّرَّ فِى ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ إِنَّهُۥ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSema: Ameyateremsha haya ajuaye siri za katika mbingu na ardhi. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالُوا۟ مَالِ هَٰذَا ٱلرَّسُولِ يَأْكُلُ ٱلطَّعَامَ وَيَمْشِى فِى ٱلْأَسْوَاقِ لَوْلَآ أُنزِلَ إِلَيْهِ مَلَكٌ فَيَكُونَ مَعَهُۥ نَذِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wakasema: Ana nini Mtume huyu? Anakula chakula, na anatembea masokoni! Mbona hakuteremshiwa Malaika akawa mwonyaji pamoja naye?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَوْ يُلْقَىٰٓ إِلَيْهِ كَنزٌ أَوْ تَكُونُ لَهُۥ جَنَّةٌ يَأْكُلُ مِنْهَا وَقَالَ ٱلظَّٰلِمُونَ إِن تَتَّبِعُونَ إِلَّا رَجُلًا مَّسْحُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu akaangushiwa hazina juu yake, au akawa na bustani ale katika hiyo? Wakasema madhalimu: Nyinyi hamumfuati ila mtu aliyerogwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱنظُرْ كَيْفَ ضَرَبُوا۟ لَكَ ٱلْأَمْثَٰلَ فَضَلُّوا۟ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ سَبِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTazama jinsi wanavyokupigia mifano. Basi wamepotea, wala hawataiweza Njia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

تَبَارَكَ ٱلَّذِىٓ إِن شَآءَ جَعَلَ لَكَ خَيْرًا مِّن ذَٰلِكَ جَنَّٰتٍ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ وَيَجْعَل لَّكَ قُصُورًۢا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmetukuka ambaye akitaka atakujalia yaliyo bora kuliko hayo, nayo ni mabustani yapitayo mito kati yake, na atakujaalia majumba ya fahari.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

بَلْ كَذَّبُوا۟ بِٱلسَّاعَةِ وَأَعْتَدْنَا لِمَن كَذَّبَ بِٱلسَّاعَةِ سَعِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBali wanaikanusha Saa (ya Kiyama). Na Sisi tumemuandalia Moto mkali kabisa huyo mwenye kuikanusha Saa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذَا رَأَتْهُم مِّن مَّكَانٍۭ بَعِيدٍ سَمِعُوا۟ لَهَا تَغَيُّظًا وَزَفِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUle Moto ukiwaona tangu mahali mbali, wao watasikia hasira yake na mngurumo wake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَآ أُلْقُوا۟ مِنْهَا مَكَانًا ضَيِّقًا مُّقَرَّنِينَ دَعَوْا۟ هُنَالِكَ ثُبُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa watakapotupwa humo mahali penye dhiki, hali wamefungwa, wataomba wafe.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَّا تَدْعُوا۟ ٱلْيَوْمَ ثُبُورًا وَٰحِدًا وَٱدْعُوا۟ ثُبُورًا كَثِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMsiombe kufa mara moja tu, bali mfe mara nyingi!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُلْ أَذَٰلِكَ خَيْرٌ أَمْ جَنَّةُ ٱلْخُلْدِ ٱلَّتِى وُعِدَ ٱلْمُتَّقُونَ كَانَتْ لَهُمْ جَزَآءً وَمَصِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSema: Je, haya ni bora au Bustani ya milele, ambayo wameahidiwa wacha Mungu, iwe kwao malipo na marejeo?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَّهُمْ فِيهَا مَا يَشَآءُونَ خَٰلِدِينَ كَانَ عَلَىٰ رَبِّكَ وَعْدًا مَّسْـُٔولًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatayapata humo wayatakayo daima dawamu. Hii ni ahadi juu ya Mola wako Mlezi, inayoombwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيَوْمَ يَحْشُرُهُمْ وَمَا يَعْبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ فَيَقُولُ ءَأَنتُمْ أَضْلَلْتُمْ عِبَادِى هَٰٓؤُلَآءِ أَمْ هُمْ ضَلُّوا۟ ٱلسَّبِيلَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa siku atakapowakusanya wao na hao wanaowaabudu, na akasema: Je, ni nyinyi mliowapoteza waja wangu hawa, au wao wenyewe walipotea njia?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ سُبْحَٰنَكَ مَا كَانَ يَنۢبَغِى لَنَآ أَن نَّتَّخِذَ مِن دُونِكَ مِنْ أَوْلِيَآءَ وَلَٰكِن مَّتَّعْتَهُمْ وَءَابَآءَهُمْ حَتَّىٰ نَسُوا۟ ٱلذِّكْرَ وَكَانُوا۟ قَوْمًۢا بُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatasema: Subhanaka! (Umetakasika na upungufu!) Haikutupasia sisi kuchukulia walinzi badala yako, lakini Wewe uliwastarehesha wao na baba zao hata wakasahau kukumbuka, na wakawa watu walioangamia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَقَدْ كَذَّبُوكُم بِمَا تَقُولُونَ فَمَا تَسْتَطِيعُونَ صَرْفًا وَلَا نَصْرًا وَمَن يَظْلِم مِّنكُمْ نُذِقْهُ عَذَابًا كَبِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi waliwakanusheni kwa mliyoyasema. Kwa hivyo hamwezi kujiondolea wala kujisaidia. Na atakayedhulumu miongoni mwenu tutamwonjesha adhabu kubwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَآ أَرْسَلْنَا قَبْلَكَ مِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ إِلَّآ إِنَّهُمْ لَيَأْكُلُونَ ٱلطَّعَامَ وَيَمْشُونَ فِى ٱلْأَسْوَاقِ وَجَعَلْنَا بَعْضَكُمْ لِبَعْضٍ فِتْنَةً أَتَصْبِرُونَ وَكَانَ رَبُّكَ بَصِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hatukuwatuma kabla yako Mitume wowote ila kwa hakika na yakini walikuwa wakila chakula, na wakienda masokoni. Na tumewajaalia baadhi yenu wawe ni majaribio kwa wengine. Je, mtasubiri? Na Mola wako Mlezi ni Mwenye kuona.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالَ ٱلَّذِينَ لَا يَرْجُونَ لِقَآءَنَا لَوْلَآ أُنزِلَ عَلَيْنَا ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ أَوْ نَرَىٰ رَبَّنَا لَقَدِ ٱسْتَكْبَرُوا۟ فِىٓ أَنفُسِهِمْ وَعَتَوْ عُتُوًّا كَبِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa walisema wale wasiotarajia kukutana nasi, "Mbona sisi hatukuteremshiwa Malaika au tumwone nasi Mola wetu Mlezi?" Hakika, hawa wamejiona bora nafsi zao; na wamepanda kichwa, vikubwa mno!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ يَرَوْنَ ٱلْمَلَٰٓئِكَةَ لَا بُشْرَىٰ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُجْرِمِينَ وَيَقُولُونَ حِجْرًا مَّحْجُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku watakapowaona Malaika, hakutakuwa na furaha yoyote siku hiyo kwa wahalifu. Na watasema, "Mwenyezi Mungu apishe mbali!"

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَدِمْنَآ إِلَىٰ مَا عَمِلُوا۟ مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَٰهُ هَبَآءً مَّنثُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tutayaendea yale waliyoyatenda katika matendo na tuyafanye kama mavumbi yaliyotawanywa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَصْحَٰبُ ٱلْجَنَّةِ يَوْمَئِذٍ خَيْرٌ مُّسْتَقَرًّا وَأَحْسَنُ مَقِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatu wa Bustanini siku hiyo watakuwa katika makazi bora na mahali penye starehe nzuri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيَوْمَ تَشَقَّقُ ٱلسَّمَآءُ بِٱلْغَمَٰمِ وَنُزِّلَ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ تَنزِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa siku zitakapopasuka mbingu zifunguke kwa mawingu, na wateremshwe Malaika kwa wingi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلْمُلْكُ يَوْمَئِذٍ ٱلْحَقُّ لِلرَّحْمَٰنِ وَكَانَ يَوْمًا عَلَى ٱلْكَٰفِرِينَ عَسِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUfalme wa haki siku hiyo utakuwa wa Arrahman (Mwingi wa rehema), na itakuwa siku ngumu kwa makafiri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيَوْمَ يَعَضُّ ٱلظَّالِمُ عَلَىٰ يَدَيْهِ يَقُولُ يَٰلَيْتَنِى ٱتَّخَذْتُ مَعَ ٱلرَّسُولِ سَبِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa siku ambayo mwenye kudhulumu atajiuma mikono yake, na huku anasema: Laiti ningelishika njia pamoja na Mtume!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَٰوَيْلَتَىٰ لَيْتَنِى لَمْ أَتَّخِذْ فُلَانًا خَلِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterEwe ole wangu! Laiti nisingelimfanya fulani kuwa rafiki mwandani!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَّقَدْ أَضَلَّنِى عَنِ ٱلذِّكْرِ بَعْدَ إِذْ جَآءَنِى وَكَانَ ٱلشَّيْطَٰنُ لِلْإِنسَٰنِ خَذُولًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika alinipoteza, nikaacha Ukumbusho, baada ya kwisha nijia, na kweli Shetani ni haini mkubwa kwa mwanadamu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالَ ٱلرَّسُولُ يَٰرَبِّ إِنَّ قَوْمِى ٱتَّخَذُوا۟ هَٰذَا ٱلْقُرْءَانَ مَهْجُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa Mtume alikuwa akisema: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika kaumu yangu wameifanya hii Qur-ani kuwa ni kihame.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَا لِكُلِّ نَبِىٍّ عَدُوًّا مِّنَ ٱلْمُجْرِمِينَ وَكَفَىٰ بِرَبِّكَ هَادِيًا وَنَصِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa vivyo hivyo tumemfanyia kila Nabii adui miongoni mwa wahalifu, na Mola wako Mlezi anatosha kuwa Mwenye kuongoa na Mwenye kunusuru.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَوْلَا نُزِّلَ عَلَيْهِ ٱلْقُرْءَانُ جُمْلَةً وَٰحِدَةً كَذَٰلِكَ لِنُثَبِّتَ بِهِۦ فُؤَادَكَ وَرَتَّلْنَٰهُ تَرْتِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wakasema wale waliokufuru: Kwa nini hakuteremshiwa Qur-ani yote mara moja tu? Hayo ni hivyo ili tuuimarishe kwayo (ufahamu wa) moyo wako, na ndiyo tumeisoma kwa mafungu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَا يَأْتُونَكَ بِمَثَلٍ إِلَّا جِئْنَٰكَ بِٱلْحَقِّ وَأَحْسَنَ تَفْسِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWala hawatakuletea mfano wowote, isipokuwa na Sisi tutakuletea (jawabu) kwa haki, na tafsiri iliyo bora zaidi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِينَ يُحْشَرُونَ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ إِلَىٰ جَهَنَّمَ أُو۟لَٰٓئِكَ شَرٌّ مَّكَانًا وَأَضَلُّ سَبِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWale ambao watakusanywa kwa nyuso zao hadi katika Jahannamu, hao watakuwa na mahali pabaya mno, nao ndio wenye kuipotea zaidi njia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ ءَاتَيْنَا مُوسَى ٱلْكِتَٰبَ وَجَعَلْنَا مَعَهُۥٓ أَخَاهُ هَٰرُونَ وَزِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika tulimpa Musa Kitabu na tukamuweka pamoja naye kakaye, Harun, kuwa msaidizi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَقُلْنَا ٱذْهَبَآ إِلَى ٱلْقَوْمِ ٱلَّذِينَ كَذَّبُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا فَدَمَّرْنَٰهُمْ تَدْمِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTukawaambia: "Nendeni kwa kaumu waliokanusha Ishara zetu." Basi tukawateketeza kabisa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَوْمَ نُوحٍ لَّمَّا كَذَّبُوا۟ ٱلرُّسُلَ أَغْرَقْنَٰهُمْ وَجَعَلْنَٰهُمْ لِلنَّاسِ ءَايَةً وَأَعْتَدْنَا لِلظَّٰلِمِينَ عَذَابًا أَلِيمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kaumu ya Nuhu, walipowakanusha Mitume, tuliwazamisha, na tukawafanya ni Ishara kwa watu. Na tumewaandalia madhalimu adhabu chungu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَعَادًا وَثَمُودَا۟ وَأَصْحَٰبَ ٱلرَّسِّ وَقُرُونًۢا بَيْنَ ذَٰلِكَ كَثِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa (tuliwaangamiza) kina 'Adi na Thamudi na watu wa Rass na vizazi vingi vilivyokuwa kati yao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَكُلًّا ضَرَبْنَا لَهُ ٱلْأَمْثَٰلَ وَكُلًّا تَبَّرْنَا تَتْبِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wote tuliwapigia mifano, na wote tuliwaangamiza kabisa kabisa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ أَتَوْا۟ عَلَى ٱلْقَرْيَةِ ٱلَّتِىٓ أُمْطِرَتْ مَطَرَ ٱلسَّوْءِ أَفَلَمْ يَكُونُوا۟ يَرَوْنَهَا بَلْ كَانُوا۟ لَا يَرْجُونَ نُشُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa yakini wao walikwisha ujia mji ulioteremshiwa mvua mbaya. Basi, je, hawakuwa wakiuona? Bali walikuwa hawataraji kufufuliwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَا رَأَوْكَ إِن يَتَّخِذُونَكَ إِلَّا هُزُوًا أَهَٰذَا ٱلَّذِى بَعَثَ ٱللَّهُ رَسُولًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wanapokuona, hawakuchukulii isipokuwa ni mzaha tu, na (wanasema): Ati huyu ndiye Mwenyezi Mungu alimtuma kuwa Mtume?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِن كَادَ لَيُضِلُّنَا عَنْ ءَالِهَتِنَا لَوْلَآ أَن صَبَرْنَا عَلَيْهَا وَسَوْفَ يَعْلَمُونَ حِينَ يَرَوْنَ ٱلْعَذَابَ مَنْ أَضَلُّ سَبِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa hakika alikuwa karibu zaidi kutupoteza tuiache miungu yetu, lau kuwa hatukushikamana nayo kwa kuvumilia. Bado watakuja jua, watakapoiona adhabu, ni nani aliyepotea zaidi njia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَرَءَيْتَ مَنِ ٱتَّخَذَ إِلَٰهَهُۥ هَوَىٰهُ أَفَأَنتَ تَكُونُ عَلَيْهِ وَكِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, umemwona aliyeyafanya matamanio yake kuwa ndiyo mungu wake? Basi je, wewe utakuwa ni wakili wake?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ تَحْسَبُ أَنَّ أَكْثَرَهُمْ يَسْمَعُونَ أَوْ يَعْقِلُونَ إِنْ هُمْ إِلَّا كَٱلْأَنْعَٰمِ بَلْ هُمْ أَضَلُّ سَبِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wewe unadhani kwamba wengi wao wanasikia au wanaelewa? Hao sio isipokuwa ni kama wanyama tu, bali wao wamepotea zaidi njia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَلَمْ تَرَ إِلَىٰ رَبِّكَ كَيْفَ مَدَّ ٱلظِّلَّ وَلَوْ شَآءَ لَجَعَلَهُۥ سَاكِنًا ثُمَّ جَعَلْنَا ٱلشَّمْسَ عَلَيْهِ دَلِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, huoni jinsi Mola wako Mlezi anavyokitandaza kivuli. Na angelitaka, angelikifanya kikatulia tu. Kisha tumelifanya jua kuwa ni kiongozi wake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ثُمَّ قَبَضْنَٰهُ إِلَيْنَا قَبْضًا يَسِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKisha tunakivutia kwetu kidogo kidogo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَهُوَ ٱلَّذِى جَعَلَ لَكُمُ ٱلَّيْلَ لِبَاسًا وَٱلنَّوْمَ سُبَاتًا وَجَعَلَ ٱلنَّهَارَ نُشُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNaye ndiye aliyewafanyia usiku kuwa ni vazi, na usingizi kuwa mapumziko, na akawafanyia mchana ni kufufuka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَهُوَ ٱلَّذِىٓ أَرْسَلَ ٱلرِّيَٰحَ بُشْرًۢا بَيْنَ يَدَىْ رَحْمَتِهِۦ وَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً طَهُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNaye ndiye anayezituma pepo kuwa bishara njema kabla ya rehema yake, na tunayateremsha kutoka mbinguni maji safi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لِّنُحْـِۧىَ بِهِۦ بَلْدَةً مَّيْتًا وَنُسْقِيَهُۥ مِمَّا خَلَقْنَآ أَنْعَٰمًا وَأَنَاسِىَّ كَثِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIli kwa hayo tuihuishe nchi iliyokufa, na tuwanyweshe wanyama na watu wengi tuliowaumba.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ صَرَّفْنَٰهُ بَيْنَهُمْ لِيَذَّكَّرُوا۟ فَأَبَىٰٓ أَكْثَرُ ٱلنَّاسِ إِلَّا كُفُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa yakini tumeibadilibadili kati yao wapate kukumbuka. Lakini wengi wa watu wanakataa isipokuwa kukufuru tu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَوْ شِئْنَا لَبَعَثْنَا فِى كُلِّ قَرْيَةٍ نَّذِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tungelitaka, tungelituma katika kila mji Mwonyaji.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلَا تُطِعِ ٱلْكَٰفِرِينَ وَجَٰهِدْهُم بِهِۦ جِهَادًا كَبِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi usiwatii makafiri. Na pambana nao kwayo kwa Jihadi kubwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَهُوَ ٱلَّذِى مَرَجَ ٱلْبَحْرَيْنِ هَٰذَا عَذْبٌ فُرَاتٌ وَهَٰذَا مِلْحٌ أُجَاجٌ وَجَعَلَ بَيْنَهُمَا بَرْزَخًا وَحِجْرًا مَّحْجُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNaye ndiye aliyezipeleka bahari mbili, hii ni tamu mno, na hii ni ya chumvi chungu. Na akaweka baina yake kinga na kizuizi kizuiacho.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَهُوَ ٱلَّذِى خَلَقَ مِنَ ٱلْمَآءِ بَشَرًا فَجَعَلَهُۥ نَسَبًا وَصِهْرًا وَكَانَ رَبُّكَ قَدِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNaye ndiye aliyemuumba mwanadamu kutokana na maji, akamjaalia kuwa na nasaba na ushemeji. Na Mola wako Mlezi ni Muweza mno.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيَعْبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَنفَعُهُمْ وَلَا يَضُرُّهُمْ وَكَانَ ٱلْكَافِرُ عَلَىٰ رَبِّهِۦ ظَهِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wanayaabudu badala ya Mwenyezi Mungu yasiyowafaa wala yasiyowadhuru. Na kafiri daima ni msaidizi wa kumpinga Mola wake Mlezi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَآ أَرْسَلْنَٰكَ إِلَّا مُبَشِّرًا وَنَذِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNasi hatukukutuma isipokuwa uwe Mbashiri na Mwonyaji.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُلْ مَآ أَسْـَٔلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِلَّا مَن شَآءَ أَن يَتَّخِذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSema: Sikuwaomba ujira wowote juu yake; isipokuwa atakaye na ashike njia iendayo kwa Mola wake Mlezi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَتَوَكَّلْ عَلَى ٱلْحَىِّ ٱلَّذِى لَا يَمُوتُ وَسَبِّحْ بِحَمْدِهِۦ وَكَفَىٰ بِهِۦ بِذُنُوبِ عِبَادِهِۦ خَبِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mtegemee aliye Hai, ambaye hafi. Na umtakase kwa sifa zake. Naye anatosha kuwa ndiye Mwenye habari zote za dhambi za waja wake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِى سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ ٱسْتَوَىٰ عَلَى ٱلْعَرْشِ ٱلرَّحْمَٰنُ فَسْـَٔلْ بِهِۦ خَبِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbaye aliziumba mbingu na ardhi, na vilivyo kati yake kwa siku sita. Kisha akainuka akawa juu ya Kiti cha Enzi. Mwingi wa rehema (Arrahman)! Uliza habari zake kwa amjuaye.[1]

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱسْجُدُوا۟ لِلرَّحْمَٰنِ قَالُوا۟ وَمَا ٱلرَّحْمَٰنُ أَنَسْجُدُ لِمَا تَأْمُرُنَا وَزَادَهُمْ نُفُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wanapoambiwa: Msujudieni Arrahman (Mwingi wa rehema!) Wao husema: Ni nani Arrahman (Mwingi wa rehema)? Je, tumsujudie unayetuamrisha wewe tu? Na huwazidishia kujitenga mbali.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

تَبَارَكَ ٱلَّذِى جَعَلَ فِى ٱلسَّمَآءِ بُرُوجًا وَجَعَلَ فِيهَا سِرَٰجًا وَقَمَرًا مُّنِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNi Mwenye baraka nyingi yule aliyezijalia nyota mbinguni, na akajalia humo taa na mwezi unaong'ara.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَهُوَ ٱلَّذِى جَعَلَ ٱلَّيْلَ وَٱلنَّهَارَ خِلْفَةً لِّمَنْ أَرَادَ أَن يَذَّكَّرَ أَوْ أَرَادَ شُكُورًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNaye ndiye aliyefanya usiku na mchana kufuatana kwa nafuu ya yule anayetaka kukumbuka, au anayetaka kushukuru.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَعِبَادُ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى ٱلْأَرْضِ هَوْنًا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ ٱلْجَٰهِلُونَ قَالُوا۟ سَلَٰمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa waja wa Arrahman (Mwingi wa rehema) ni wale wanaotembea ulimwenguni kwa staha, na wajinga wakiwasemeza, hujibu: Salama!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ يَبِيتُونَ لِرَبِّهِمْ سُجَّدًا وَقِيَٰمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale wanaokesha kwa ajili ya Mola wao Mlezi kwa kusujudu na kusimama.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا ٱصْرِفْ عَنَّا عَذَابَ جَهَنَّمَ إِنَّ عَذَابَهَا كَانَ غَرَامًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale wanaosema: "Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu ya Jahannamu. Hakika adhabu yake ikimpata mtu haimwachi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّهَا سَآءَتْ مُسْتَقَرًّا وَمُقَامًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika hiyo ni kituo na makao mabaya."

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ إِذَآ أَنفَقُوا۟ لَمْ يُسْرِفُوا۟ وَلَمْ يَقْتُرُوا۟ وَكَانَ بَيْنَ ذَٰلِكَ قَوَامًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale ambao wanapotoa matumizi, hawatumii kwa fujo wala hawafanyi ubahili, bali wanakuwa katikati baina ya hayo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ وَلَا يَقْتُلُونَ ٱلنَّفْسَ ٱلَّتِى حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ يَلْقَ أَثَامًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale wasiomuomba mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu, wala hawaui nafsi aliyoiharimisha Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa haki, wala hawazini. Na atakayefanya hayo, atapata madhara.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يُضَٰعَفْ لَهُ ٱلْعَذَابُ يَوْمَ ٱلْقِيَٰمَةِ وَيَخْلُدْ فِيهِۦ مُهَانًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAtazidishiwa adhabu Siku ya Kiyama, na atadumu humo kwa kufedheheshwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِلَّا مَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَٰلِحًا فَأُو۟لَٰٓئِكَ يُبَدِّلُ ٱللَّهُ سَيِّـَٔاتِهِمْ حَسَنَٰتٍ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورًا رَّحِيمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIsipokuwa atakayetubu, na akaamini, na akatenda matendo mema. Basi hao Mwenyezi Mungu atayabadilisha maovu yao yawe mema. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَن تَابَ وَعَمِلَ صَٰلِحًا فَإِنَّهُۥ يَتُوبُ إِلَى ٱللَّهِ مَتَابًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa aliyetubu na akafanya mema, basi hakika huyo ametubu kweli kweli kwa Mwenyezi Mungu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ لَا يَشْهَدُونَ ٱلزُّورَ وَإِذَا مَرُّوا۟ بِٱللَّغْوِ مَرُّوا۟ كِرَامًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale ambao hawatoi ushahidi wa uongo, na pindi wapitapo penye upuuzi, hupita kwa heshima yao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُوا۟ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمْ لَمْ يَخِرُّوا۟ عَلَيْهَا صُمًّا وَعُمْيَانًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale ambao wanapokumbushwa Ishara za Mola wao Mlezi hawajifanyi viziwi nazo, na vipofu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَٰجِنَا وَذُرِّيَّٰتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَٱجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale wanaosema: "Mola wetu Mlezi! Tupe katika wake zetu na wana wetu yaburudishayo macho, na utujalie tuwe waongozi kwa wacha Mungu."

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أُو۟لَٰٓئِكَ يُجْزَوْنَ ٱلْغُرْفَةَ بِمَا صَبَرُوا۟ وَيُلَقَّوْنَ فِيهَا تَحِيَّةً وَسَلَٰمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHao ndio watakaolipwa makao ya juu kwa kuwa walisubiri, na watakuta humo maamkizi na salama.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

خَٰلِدِينَ فِيهَا حَسُنَتْ مُسْتَقَرًّا وَمُقَامًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWadumu humo, kituo na makao mazuri kabisa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُلْ مَا يَعْبَؤُا۟ بِكُمْ رَبِّى لَوْلَا دُعَآؤُكُمْ فَقَدْ كَذَّبْتُمْ فَسَوْفَ يَكُونُ لِزَامًۢا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSema: Mola wangu Mlezi asingewajali lau kuwa si kuomba kwenu. Lakini nyinyi mmemkadhibisha. Basi adhabu lazima iwe.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70