Mwanzo › Sura › Sura Al-Hijr
Sura Al-Hijr الحجر
Aya 99 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 54
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ الٓر تِلْكَ ءَايَٰتُ ٱلْكِتَٰبِ وَقُرْءَانٍ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alif Lam Ra.[1] Hizi ni Aya za Kitabu na Qur-ani inayobainisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
رُّبَمَا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَوْ كَانُوا۟ مُسْلِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Huenda ikawa wale waliokufuru wakatamani kwamba wangekuwa Waislamu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ذَرْهُمْ يَأْكُلُوا۟ وَيَتَمَتَّعُوا۟ وَيُلْهِهِمُ ٱلْأَمَلُ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Waache wale, na wastarehe, na yawazuge matumaini. Basi watakujajua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٌ مَّعْلُومٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hatukuuangamiza mji wowote ule isipokuwa ulikuwa na muda wake maalumu ulioandikiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَّا تَسْبِقُ مِنْ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسْتَـْٔخِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hawawezi umma wowote kuutangulia muda wao, wala kuchelewa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقَالُوا۟ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِى نُزِّلَ عَلَيْهِ ٱلذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na walisema, "Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَّوْ مَا تَأْتِينَا بِٱلْمَلَٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli?"
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَا نُنَزِّلُ ٱلْمَلَٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَمَا كَانُوٓا۟ إِذًا مُّنظَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Sisi hatuwateremshi Malaika isipokuwa kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا ٱلذِّكْرَ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi ndio tuliouteremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutakaoulinda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ فِى شِيَعِ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika tulikwishatuma Mitume kabla yako kwa mataifa ya mwanzo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakuwajia Mtume yeyote isipokuwa walikuwa wakimfanyia stihizai.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَٰلِكَ نَسْلُكُهُۥ فِى قُلُوبِ ٱلْمُجْرِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kama hivi ndivyo tunavyoyaingiza katika nyoyo za wahalifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِۦ وَقَدْ خَلَتْ سُنَّةُ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hawayaamini haya, na ilhali imekwishawapitia desturi ya wa mwanzo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَوْ فَتَحْنَا عَلَيْهِم بَابًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَظَلُّوا۟ فِيهِ يَعْرُجُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na lau tungeliwafungulia mlango huko mbinguni, wakawa wanapanda kupitia humo,
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَقَالُوٓا۟ إِنَّمَا سُكِّرَتْ أَبْصَٰرُنَا بَلْ نَحْنُ قَوْمٌ مَّسْحُورُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wangelisema: Hakika macho yetu yameleweshwa tu. Bali sisi wenyewe ni kaumu tuliofanyiwa uchawi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ جَعَلْنَا فِى ٱلسَّمَآءِ بُرُوجًا وَزَيَّنَّٰهَا لِلنَّٰظِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَحَفِظْنَٰهَا مِن كُلِّ شَيْطَٰنٍ رَّجِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tumezilinda kutokana na kila shetani aliyelaaniwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا مَنِ ٱسْتَرَقَ ٱلسَّمْعَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kilicho dhahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلْأَرْضَ مَدَدْنَٰهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَٰسِىَ وَأَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَىْءٍ مَّوْزُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ardhi tumeitandaza, na humo tumeweka milima madhubuti, na tumeotesha ndani yake katika kila kitu kwa kiasi chake.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَعَلْنَا لَكُمْ فِيهَا مَعَٰيِشَ وَمَن لَّسْتُمْ لَهُۥ بِرَٰزِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tumewafanyia humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِن مِّن شَىْءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَآئِنُهُۥ وَمَا نُنَزِّلُهُۥٓ إِلَّا بِقَدَرٍ مَّعْلُومٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi isipokuwa kwa kipimo maalumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَرْسَلْنَا ٱلرِّيَٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلْنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً فَأَسْقَيْنَٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمْ لَهُۥ بِخَٰزِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayoyaweka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّا لَنَحْنُ نُحْىِۦ وَنُمِيتُ وَنَحْنُ ٱلْوَٰرِثُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Sisi ndio tunaohuisha na tunaofisha. Na Sisi ndio Warithi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ عَلِمْنَا ٱلْمُسْتَقْدِمِينَ مِنكُمْ وَلَقَدْ عَلِمْنَا ٱلْمُسْتَـْٔخِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika tunawajua waliotangulia katika nyinyi, na tunawajua waliobaki nyuma.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحْشُرُهُمْ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakayewakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua mno.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ مِن صَلْصَٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika tulimuumba Mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلْجَآنَّ خَلَقْنَٰهُ مِن قَبْلُ مِن نَّارِ ٱلسَّمُومِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Naye Jini tulimuumba hapo kabla kutokana na moto wa upepo umoto.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَٰٓئِكَةِ إِنِّى خَٰلِقٌۢ بَشَرًا مِّن صَلْصَٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Mola wako Mlezi alipowaambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِذَا سَوَّيْتُهُۥ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِى فَقَعُوا۟ لَهُۥ سَٰجِدِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi nitakapomtengeneza sawasawa, na nikampulizia katika roho yangu, basi angukeni kumsujudia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَسَجَدَ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi Malaika wote pamoja walimsujudia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّآ إِبْلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ يَٰٓإِبْلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ لَمْ أَكُن لِّأَسْجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقْتَهُۥ مِن صَلْصَٰلٍ مِّنْ حَمَإٍ مَّسْنُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliyemuumba kutokana na udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ فَٱخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umefukuziliwa mbali!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ عَلَيْكَ ٱللَّعْنَةَ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلدِّينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِىٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakapofufuliwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلْمُنظَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika waliopewa muhula.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْوَقْتِ ٱلْمَعْلُومِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mpaka siku ya wakati maalumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغْوَيْتَنِى لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمْ فِى ٱلْأَرْضِ وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyokuwa umenipoteza, basi hakika nitawapambia katika dunia na hakika nitawapoteza wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ ٱلْمُخْلَصِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa waja wako walioteuliwa miongoni mwao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ هَٰذَا صِرَٰطٌ عَلَىَّ مُسْتَقِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Hii ni njia ya kujia kwangu iliyonyooka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ عِبَادِى لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلْغَاوِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipokuwa wale watakaokufuata miongoni mwa wapotovu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوْعِدُهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Jahannamu ndipo mahali pao walipoahidiwa wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَهَا سَبْعَةُ أَبْوَٰبٍ لِّكُلِّ بَابٍ مِّنْهُمْ جُزْءٌ مَّقْسُومٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ina milango saba; kila mlango ulitengewa sehemu miongoni mwao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na chemchemi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱدْخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ءَامِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Wataambiwa:) Ingieni humo kwa salama na amani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَزَعْنَا مَا فِى صُدُورِهِم مِّنْ غِلٍّ إِخْوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَٰبِلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tutaondoa chuki iliyokuwa vifuani mwao, wawe ndugu, juu ya viti vya kifahari huku wameelekeana.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَا يَمَسُّهُمْ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنْهَا بِمُخْرَجِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Humo hayatawagusa machovu, wala hawatatolewa humo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
نَبِّئْ عِبَادِىٓ أَنِّىٓ أَنَا ٱلْغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wape habari waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe zaidi, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَنَّ عَذَابِى هُوَ ٱلْعَذَابُ ٱلْأَلِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwamba adhabu yangu ndiyo adhabu iliyo chungu!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَبِّئْهُمْ عَن ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wape habari za wageni wa Ibrahim.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَٰمًا قَالَ إِنَّا مِنكُمْ وَجِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Walipoingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunawaogopa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ لَا تَوْجَلْ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Usiogope. Hakika, Sisi tunakubashiria kijana mwenye elimu mno.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ أَبَشَّرْتُمُونِى عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِىَ ٱلْكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi ni kwa njia gani mnanibashiria?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ بَشَّرْنَٰكَ بِٱلْحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلْقَٰنِطِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Tunakubashiria kwa haki, basi usiwe miongoni mwa wanaokata tamaa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ وَمَن يَقْنَطُ مِن رَّحْمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Na ni nani anayekata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi isipokuwa wapotovu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Hebu mna jambo gani, enyi wajumbe?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wahalifu!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa watu wa familia ya Lut'. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا ٱمْرَأَتَهُۥ قَدَّرْنَآ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلْغَٰبِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa mkewe. Tumekwishapitisha kwamba huyo hakika atakuwa miongoni mwa watakaosalia nyuma.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلْمُرْسَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wajumbe hao walipowajia watu wa familia ya Lut'.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ إِنَّكُمْ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Lut') Alisema: Hakika nyinyi ni kaumu msiojulikana.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ بَلْ جِئْنَٰكَ بِمَا كَانُوا۟ فِيهِ يَمْتَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyokuwa wakiyafanyia shaka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَتَيْنَٰكَ بِٱلْحَقِّ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tumekujia kwa Haki, na hakika sisi ni wakweli.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَسْرِ بِأَهْلِكَ بِقِطْعٍ مِّنَ ٱلَّيْلِ وَٱتَّبِعْ أَدْبَٰرَهُمْ وَلَا يَلْتَفِتْ مِنكُمْ أَحَدٌ وَٱمْضُوا۟ حَيْثُ تُؤْمَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ondoka na ahali zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende huko mnakoamrishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقَضَيْنَآ إِلَيْهِ ذَٰلِكَ ٱلْأَمْرَ أَنَّ دَابِرَ هَٰٓؤُلَآءِ مَقْطُوعٌ مُّصْبِحِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa amekwishakatiliwa mbali.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَآءَ أَهْلُ ٱلْمَدِينَةِ يَسْتَبْشِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wakaja watu wa mji huo huku wamefurahi mno.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ ضَيْفِى فَلَا تَفْضَحُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Hakika hawa ni wageni wangu. Basi msinifedheheshe.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱتَّقُوا۟ ٱللَّهَ وَلَا تُخْزُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ أَوَلَمْ نَنْهَكَ عَنِ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Kwani hatukukukataza (kuwakaribisha) walimwengu hawa?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ هَٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِىٓ إِن كُنتُمْ فَٰعِلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema, "Hawa binti zangu (waoeni)[1], ikiwa nyinyi ni watendaji."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَعَمْرُكَ إِنَّهُمْ لَفِى سَكْرَتِهِمْ يَعْمَهُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ninaapa kwa uhai wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّيْحَةُ مُشْرِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَجَعَلْنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن سِجِّيلٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa hivyo, tukaugeuza mji huo juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa kutoka Motoni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَٰتٍ لِّلْمُتَوَسِّمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika katika hayo zipo ishara kwa wanaotafakari na kuzingatia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٍ مُّقِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika miji hii ipo kwenye njia wazi inayopitiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَةً لِّلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِن كَانَ أَصْحَٰبُ ٱلْأَيْكَةِ لَظَٰلِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika watu wa Kichakani walikuwa madhalimu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱنتَقَمْنَا مِنْهُمْ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٍ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa hivyo tukawaadhibu. Na hakika miji miwili hii iko kwenye njia iliyo wazi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ كَذَّبَ أَصْحَٰبُ ٱلْحِجْرِ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka wakazi wa Hijr waliwakadhibisha Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَءَاتَيْنَٰهُمْ ءَايَٰتِنَا فَكَانُوا۟ عَنْهَا مُعْرِضِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tuliwaletea ishara zetu, nao wakawa wanazipa migongo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَكَانُوا۟ يَنْحِتُونَ مِنَ ٱلْجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّيْحَةُ مُصْبِحِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَمَآ أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hayakuwafaa yale waliyokuwa wakiyachuma.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا خَلَقْنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَآ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَـَٔاتِيَةٌ فَٱصْفَحِ ٱلصَّفْحَ ٱلْجَمِيلَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyo kati yake isipokuwa kwa haki. Na hakika Saa ya Kiyama itafika. Basi samehe msamaha mzuri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلْخَلَّٰقُ ٱلْعَلِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji, Mwenye kujua zaidi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ ءَاتَيْنَٰكَ سَبْعًا مِّنَ ٱلْمَثَانِى وَٱلْقُرْءَانَ ٱلْعَظِيمَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika tumekupa (aya) saba zinazosomwa mara kwa mara, na Qur-ani Tukufu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَا تَمُدَّنَّ عَيْنَيْكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعْنَا بِهِۦٓ أَزْوَٰجًا مِّنْهُمْ وَلَا تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَٱخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kamwe usivinyoshee macho yako vitu tulivyowastarehesha kwavyo makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقُلْ إِنِّىٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلْمُبِينُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na sema: Hakika mimi ndiye mwonyaji mwenye kubainisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَمَآ أَنزَلْنَا عَلَى ٱلْمُقْتَسِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kama hivyo tuliwateremshia waliogawa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلَّذِينَ جَعَلُوا۟ ٱلْقُرْءَانَ عِضِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ambao waliifanya Qur-ani vipande vipande.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَوَرَبِّكَ لَنَسْـَٔلَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ninaapa kwa Mola wako Mlezi! Lazima tutawauliza wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
عَمَّا كَانُوا۟ يَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kuhusu yale waliyokuwa wakiyatenda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱصْدَعْ بِمَا تُؤْمَرُ وَأَعْرِضْ عَنِ ٱلْمُشْرِكِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wewe yadhihirishe yale uliyoamrishwa, na jitenge mbali na washirikina.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا كَفَيْنَٰكَ ٱلْمُسْتَهْزِءِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tunatosha kukukinga kutokana na wanaofanya stihizai.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلَّذِينَ يَجْعَلُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ambao wanafanya mungu mwingine kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi watakujajua!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ نَعْلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدْرُكَ بِمَا يَقُولُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ ٱلسَّٰجِدِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu, na uwe miongoni mwa wanaomsujudia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ ٱلْيَقِينُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
← Sura Ibrahim
Sura An-Nahl →
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
→
Matini ya Kiarabu na tafsiri kupitia Tanzil na QuranEnc — kama zilivyo, bila kubadilishwa · Tafsiri ni mali ya watafsiri wake na si Qur'ani yenyewe
Hii ni nyenzo ya utafiti, si chanzo cha fatwa.