Mwanzo › Sura › Sura As-Saaffaat
Sura As-Saaffaat الصافات
Aya 182 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 56
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفًّا
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ninaapa kwa wanaojipanga kwa safu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجْرًا
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwa wenye kukataza mabaya.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكْرًا
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَٰحِدٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ ٱلْمَشَٰرِقِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yake, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنْيَا بِزِينَةٍ ٱلْكَوَاكِبِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَٰنٍ مَّارِدٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kulinda na kila shetani muasi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلْمَلَإِ ٱلْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
دُحُورًا وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا مَنْ خَطِفَ ٱلْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُۥ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinachong'ara.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَآ إِنَّا خَلَقْنَٰهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍۭ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bali unastaajabu, na wao wanafanya masihara.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذَا ذُكِّرُوا۟ لَا يَذْكُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wanapokumbushwa, hawakumbuki.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذَا رَأَوْا۟ ءَايَةً يَسْتَسْخِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wanapoona Ishara, wanafanya masihara.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقَالُوٓا۟ إِنْ هَٰذَآ إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na husema: Haya si chochote isipokuwa ni uchawi tu ulio dhahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلْأَوَّلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hata baba zetu wa zamani?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَٰخِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِنَّمَا هِىَ زَجْرَةٌ وَٰحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndipo wataona!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقَالُوا۟ يَٰوَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ ٱلدِّينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
هَٰذَا يَوْمُ ٱلْفَصْلِ ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyokuwa mkiikadhibisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱحْشُرُوا۟ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ وَأَزْوَٰجَهُمْ وَمَا كَانُوا۟ يَعْبُدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakusanyeni wale waliodhulumu, na wote walio mfano wao, na hao ambao wao walikuwa wakiwaabudu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلْجَحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقِفُوهُمْ إِنَّهُم مَّسْـُٔولُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mna nini? Mbona hamsaidiani?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بَلْ هُمُ ٱلْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bali hii leo, watasalimu amri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wataelekeana wao kwa wao kuulizana.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ ٱلْيَمِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ بَل لَّمْ تَكُونُوا۟ مُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَٰنٍۭ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَٰغِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَآ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَغْوَيْنَٰكُمْ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِى ٱلْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِٱلْمُجْرِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hivyo ndivyo tutakavyowafanyia wahalifu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُمْ كَانُوٓا۟ إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wao walipokuwa wakiambiwa, "La ilaha illallaahu (Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu)", wanajivuna.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓا۟ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍۭ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بَلْ جَآءَ بِٱلْحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bali huyu amekuja kwa haki, na amewasadikisha Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّكُمْ لَذَآئِقُوا۟ ٱلْعَذَابِ ٱلْأَلِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala hamlipwi isipokuwa hayo mliyokuwa mkiyafanya.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu walioteuliwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أُو۟لَٰٓئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hao ndio watakaopata riziki maalumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكْرَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Matunda, nao wataheshimiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فِى جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Katika Bustani za neema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَٰبِلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wako juu ya viti mfano wa kitanda wameelekeana.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍۭ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchemi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بَيْضَآءَ لَذَّةٍ لِّلشَّٰرِبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَعِندَهُمْ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرْفِ عِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha, mazuri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hao wanawake kama mayai yaliyohifadhika.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wakaelekeana kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ قَآئِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّى كَانَ لِى قَرِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nilikuwa na rafiki.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُصَدِّقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Aliyekuwa akiniambia: Hivyo wewe ni katika wanaosadiki.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ati tukishakufa tukawa udongo na mafupa, ndiyo tutalipwa na kufanyiwa hesabu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Atasema: Je, nyie mnawaona?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِى سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Atasema: Wallahi! (Naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu) Ulikaribia sana kunipoteza.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّى لَكُنتُ مِنَ ٱلْمُحْضَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa waliohudhurishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, sisi hatutakufa?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا مَوْتَتَنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ ٱلْعَٰمِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa mfano wa haya na watende watendao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, kukaribishwa hivi si ndiyo bora, au mti wa Zaqqum?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا جَعَلْنَٰهَا فِتْنَةً لِّلظَّٰلِمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa waliodhulumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِىٓ أَصْلِ ٱلْجَحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika huo ni mti unaotoka katikati ya Jahannamu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
طَلْعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mashada ya matunda yake kama kwamba ni vichwa vya mashetani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِنَّهُمْ لَـَٔاكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِـُٔونَ مِنْهَا ٱلْبُطُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo kwayo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji ya moto yaliyochemka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى ٱلْجَحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa Jahimu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا۟ ءَابَآءَهُمْ ضَآلِّينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَهُمْ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمْ يُهْرَعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱنظُرْ كَيْفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلْمُنذَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walioonywa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ نَادَىٰنَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ ٱلْمُجِيبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Nuhu alituita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥ مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلْبَاقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tuliwajaalia dhuria zake ndio wenye kubakia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukamwachia (sifa njema) kwa waliokuja baadaye.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِى ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ أَغْرَقْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha tukawazamisha wale wengine.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبْرَٰهِيمَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipomjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِۦ مَاذَا تَعْبُدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَئِفْكًا ءَالِهَةً دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?"
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِى ٱلنُّجُومِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَقَالَ إِنِّى سَقِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَتَوَلَّوْا۟ عَنْهُ مُدْبِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mna nini hata hamsemi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًۢا بِٱلْيَمِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَقْبَلُوٓا۟ إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wakamjia upesi upesi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyovichonga wenyewe?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliyekuumbeni nyinyi na hivyo mnavyovifanya!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ ٱبْنُوا۟ لَهُۥ بُنْيَٰنًا فَأَلْقُوهُ فِى ٱلْجَحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَرَادُوا۟ بِهِۦ كَيْدًا فَجَعَلْنَٰهُمُ ٱلْأَسْفَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini zaidi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَقَالَ إِنِّى ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّى سَيَهْدِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
رَبِّ هَبْ لِى مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَبَشَّرْنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعْىَ قَالَ يَٰبُنَىَّ إِنِّىٓ أَرَىٰ فِى ٱلْمَنَامِ أَنِّىٓ أَذْبَحُكَ فَٱنظُرْ مَاذَا تَرَىٰ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفْعَلْ مَا تُؤْمَرُ سَتَجِدُنِىٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi alipofika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa, utanikuta mimi, Insha Allah (Mwenyezi Mungu akipenda), katika wanaosubiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَمَّآ أَسْلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلْجَبِينِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَٰدَيْنَٰهُ أَن يَٰٓإِبْرَٰهِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tulimwita: Ewe Ibrahim!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَدْ صَدَّقْتَ ٱلرُّءْيَآ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaotenda mema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلْبَلَٰٓؤُا۟ ٱلْمُبِينُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَفَدَيْنَٰهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu waliokuja baadaye.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبْرَٰهِيمَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Iwe salama kwa Ibrahim!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَبَشَّرْنَٰهُ بِإِسْحَٰقَ نَبِيًّا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَبَٰرَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰٓ إِسْحَٰقَ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِۦ مُبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuria zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَجَّيْنَٰهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ ٱلْكَرْبِ ٱلْعَظِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَصَرْنَٰهُمْ فَكَانُوا۟ هُمُ ٱلْغَٰلِبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَءَاتَيْنَٰهُمَا ٱلْكِتَٰبَ ٱلْمُسْتَبِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَهَدَيْنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلْمُسْتَقِيمَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawaongoa kwenye njia iliyonyooka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawaachia (sifa njema) katika watu waliokuja baadaye.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Iwe salama kwa Musa na Haruni!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika wawili hao ni katika waja wetu walioamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipowaambia watu wake: Hamumchi Mungu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ ٱلْخَٰلِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِى ٱلْـَٔاخِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa waliokuja baadaye.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلْ يَاسِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Iwe salama kwa Ilyas.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِى ٱلْمُحْسِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُۥ مِنْ عِبَادِنَا ٱلْمُؤْمِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ نَجَّيْنَٰهُ وَأَهْلَهُۥٓ أَجْمَعِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا عَجُوزًا فِى ٱلْغَٰبِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ثُمَّ دَمَّرْنَا ٱلْـَٔاخَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَبِٱلَّيْلِ أَفَلَا تَعْقِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na usiku. Basi je, hamyatii akilini?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ أَبَقَ إِلَى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Alipokimbia akenda katika jahazi lililosheheni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلْمُدْحَضِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walioshindwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱلْتَقَمَهُ ٱلْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَوْلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلْمُسَبِّحِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ingelikuwa hakuwa katika wanaomtakasa Mwenyezi Mungu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَلَبِثَ فِى بَطْنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bila ya shaka angelikaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَنَبَذْنَٰهُ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَنۢبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukauotesha juu yake mmea wa aina ya mung'unye.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَرْسَلْنَٰهُ إِلَىٰ مِا۟ئَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَـَٔامَنُوا۟ فَمَتَّعْنَٰهُمْ إِلَىٰ حِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ ٱلْبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلْبَنُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَمْ خَلَقْنَا ٱلْمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثًا وَهُمْ شَٰهِدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَلَآ إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tazama, hakika ni kwa uzushi wao ndio wanasema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَٰذِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَصْطَفَى ٱلْبَنَاتِ عَلَى ٱلْبَنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ati amehiari watoto wa kike kuliko wanaume?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hamkumbuki?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَمْ لَكُمْ سُلْطَٰنٌ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Au mnayo hoja iliyo wazi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأْتُوا۟ بِكِتَٰبِكُمْ إِن كُنتُمْ صَٰدِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi leteni Kitabu chenu kama nyinyi ni wakweli.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَعَلُوا۟ بَيْنَهُۥ وَبَيْنَ ٱلْجِنَّةِ نَسَبًا وَلَقَدْ عَلِمَتِ ٱلْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wameweka mahusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwishajua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سُبْحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hayo wanayomsingizia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَآ أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَٰتِنِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hamwezi kuwapoteza.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ ٱلْجَحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa yule atakayeingia Motoni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلصَّآفُّونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّا لَنَحْنُ ٱلْمُسَبِّحُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika sisi ndio wenye kutakasa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِن كَانُوا۟ لَيَقُولُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na walikuwapo waliokuwa wakisema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ ٱلْأَوَّلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tungelikuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلْمُخْلَصِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bila ya shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye kumkusudia Yeye tu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكَفَرُوا۟ بِهِۦ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Lakini waliukufuru. Basi watakuja jua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu waliotumwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُمْ لَهُمُ ٱلْمَنصُورُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلْغَٰلِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi waachilie mbali kwa muda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na watazame, nao wataona.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, wanaiharakishia adhabu yetu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلْمُنذَرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na waache kwa muda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tazama, na wao wataona.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سُبْحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ametakasika Mola wako Mlezi Mwenye utukufu mbali na yale wanayomzulia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Salamu juu ya Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
← Sura Yaseen
Sura Saad →
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
→
Matini ya Kiarabu na tafsiri kupitia Tanzil na QuranEnc — kama zilivyo, bila kubadilishwa · Tafsiri ni mali ya watafsiri wake na si Qur'ani yenyewe
Hii ni nyenzo ya utafiti, si chanzo cha fatwa.