Mwanzo › Sura › Sura Yaseen
Sura Yaseen يس
Aya 83 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 41
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ يسٓ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ya Sin.[1]
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلْقُرْءَانِ ٱلْحَكِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center (Ninaapa) kwa Qur-ani yenye hekima!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّكَ لَمِنَ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika wewe ni miongoni mwa waliotumwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
عَلَىٰ صِرَٰطٍ مُّسْتَقِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Juu ya njia iliyonyooka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
تَنزِيلَ ٱلْعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لِتُنذِرَ قَوْمًا مَّآ أُنذِرَ ءَابَآؤُهُمْ فَهُمْ غَٰفِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَقَدْ حَقَّ ٱلْقَوْلُ عَلَىٰٓ أَكْثَرِهِمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا جَعَلْنَا فِىٓ أَعْنَٰقِهِمْ أَغْلَٰلًا فَهِىَ إِلَى ٱلْأَذْقَانِ فَهُم مُّقْمَحُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَعَلْنَا مِنۢ بَيْنِ أَيْدِيهِمْ سَدًّا وَمِنْ خَلْفِهِمْ سَدًّا فَأَغْشَيْنَٰهُمْ فَهُمْ لَا يُبْصِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao. Na tumewafunika macho yao, kwa hivyo hawaoni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَسَوَآءٌ عَلَيْهِمْ ءَأَنذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنذِرْهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّمَا تُنذِرُ مَنِ ٱتَّبَعَ ٱلذِّكْرَ وَخَشِىَ ٱلرَّحْمَٰنَ بِٱلْغَيْبِ فَبَشِّرْهُ بِمَغْفِرَةٍ وَأَجْرٍ كَرِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman (Mwingi wa rehema), kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا نَحْنُ نُحْىِ ٱلْمَوْتَىٰ وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا۟ وَءَاثَٰرَهُمْ وَكُلَّ شَىْءٍ أَحْصَيْنَٰهُ فِىٓ إِمَامٍ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tunawafufua wafu na tunayaandika wanayoyatanguliza, na wanayoyaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari la asili lenye kubainisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱضْرِبْ لَهُم مَّثَلًا أَصْحَٰبَ ٱلْقَرْيَةِ إِذْ جَآءَهَا ٱلْمُرْسَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wapigie mfano wa wakazi wa mji walipojiwa na Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ أَرْسَلْنَآ إِلَيْهِمُ ٱثْنَيْنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزْنَا بِثَالِثٍ فَقَالُوٓا۟ إِنَّآ إِلَيْكُم مُّرْسَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Tulipowatumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: "Hakika sisi tumetumwa kwenu."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ مَآ أَنتُمْ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَمَآ أَنزَلَ ٱلرَّحْمَٰنُ مِن شَىْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا تَكْذِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: "Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uongo tu."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ رَبُّنَا يَعْلَمُ إِنَّآ إِلَيْكُمْ لَمُرْسَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: "Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا عَلَيْنَآ إِلَّا ٱلْبَلَٰغُ ٱلْمُبِينُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوٓا۟ إِنَّا تَطَيَّرْنَا بِكُمْ لَئِن لَّمْ تَنتَهُوا۟ لَنَرْجُمَنَّكُمْ وَلَيَمَسَّنَّكُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: "Sisi hakika sisi tunaona mkosi kwenu. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ طَٰٓئِرُكُم مَّعَكُمْ أَئِن ذُكِّرْتُم بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ مُّسْرِفُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: "Mkosi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu waliopindukia mipaka."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَآءَ مِنْ أَقْصَا ٱلْمَدِينَةِ رَجُلٌ يَسْعَىٰ قَالَ يَٰقَوْمِ ٱتَّبِعُوا۟ ٱلْمُرْسَلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: "Enyi watu wangu! Wafuateni hawa waliotumwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱتَّبِعُوا۟ مَن لَّا يَسْـَٔلُكُمْ أَجْرًا وَهُم مُّهْتَدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا لِىَ لَآ أَعْبُدُ ٱلَّذِى فَطَرَنِى وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwa nini nisimuabudu yule aliyeniumba na kwake nitarejeshwa?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ءَأَتَّخِذُ مِن دُونِهِۦٓ ءَالِهَةً إِن يُرِدْنِ ٱلرَّحْمَٰنُ بِضُرٍّ لَّا تُغْنِ عَنِّى شَفَٰعَتُهُمْ شَيْـًٔا وَلَا يُنقِذُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani (Mwingi wa Rehema) akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّىٓ إِذًا لَّفِى ضَلَٰلٍ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنِّىٓ ءَامَنتُ بِرَبِّكُمْ فَٱسْمَعُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!"
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قِيلَ ٱدْخُلِ ٱلْجَنَّةَ قَالَ يَٰلَيْتَ قَوْمِى يَعْلَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Akaambiwa: "Ingia Peponi!" Akasema: "Laiti kuwa watu wangu wangelijua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بِمَا غَفَرَ لِى رَبِّى وَجَعَلَنِى مِنَ ٱلْمُكْرَمِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Jinsi Mola wangu Mlezi alivyonisamehe, na akanifanya miongoni mwa walioheshimiwa."
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَنزَلْنَا عَلَىٰ قَوْمِهِۦ مِنۢ بَعْدِهِۦ مِن جُندٍ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَمَا كُنَّا مُنزِلِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَٰحِدَةً فَإِذَا هُمْ خَٰمِدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Haukuwa ila ukelele mmoja tu, na mara walizimwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يَٰحَسْرَةً عَلَى ٱلْعِبَادِ مَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا۟ بِهِۦ يَسْتَهْزِءُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَلَمْ يَرَوْا۟ كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّنَ ٱلْقُرُونِ أَنَّهُمْ إِلَيْهِمْ لَا يَرْجِعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, hawaoni umma ngapi tulizoziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِن كُلٌّ لَّمَّا جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَءَايَةٌ لَّهُمُ ٱلْأَرْضُ ٱلْمَيْتَةُ أَحْيَيْنَٰهَا وَأَخْرَجْنَا مِنْهَا حَبًّا فَمِنْهُ يَأْكُلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Ishara hiyo kwao ni ardhi iliyokufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanakula katika hizo!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَجَعَلْنَا فِيهَا جَنَّٰتٍ مِّن نَّخِيلٍ وَأَعْنَٰبٍ وَفَجَّرْنَا فِيهَا مِنَ ٱلْعُيُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemichemi ndani yake.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لِيَأْكُلُوا۟ مِن ثَمَرِهِۦ وَمَا عَمِلَتْهُ أَيْدِيهِمْ أَفَلَا يَشْكُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ili wale katika matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سُبْحَٰنَ ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلْأَزْوَٰجَ كُلَّهَا مِمَّا تُنۢبِتُ ٱلْأَرْضُ وَمِنْ أَنفُسِهِمْ وَمِمَّا لَا يَعْلَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ametakasika yule aliyeumba dume na jike vyote katika vinavyomea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyovijua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَءَايَةٌ لَّهُمُ ٱلَّيْلُ نَسْلَخُ مِنْهُ ٱلنَّهَارَ فَإِذَا هُم مُّظْلِمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلشَّمْسُ تَجْرِى لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ذَٰلِكَ تَقْدِيرُ ٱلْعَزِيزِ ٱلْعَلِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua vyema.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلْقَمَرَ قَدَّرْنَٰهُ مَنَازِلَ حَتَّىٰ عَادَ كَٱلْعُرْجُونِ ٱلْقَدِيمِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَا ٱلشَّمْسُ يَنۢبَغِى لَهَآ أَن تُدْرِكَ ٱلْقَمَرَ وَلَا ٱلَّيْلُ سَابِقُ ٱلنَّهَارِ وَكُلٌّ فِى فَلَكٍ يَسْبَحُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَءَايَةٌ لَّهُمْ أَنَّا حَمَلْنَا ذُرِّيَّتَهُمْ فِى ٱلْفُلْكِ ٱلْمَشْحُونِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuria zao katika jahazi lililosheheni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَخَلَقْنَا لَهُم مِّن مِّثْلِهِۦ مَا يَرْكَبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyovipanda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِن نَّشَأْ نُغْرِقْهُمْ فَلَا صَرِيخَ لَهُمْ وَلَا هُمْ يُنقَذُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukitaka, tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِلَّا رَحْمَةً مِّنَّا وَمَتَٰعًا إِلَىٰ حِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Isipokuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱتَّقُوا۟ مَا بَيْنَ أَيْدِيكُمْ وَمَا خَلْفَكُمْ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wanapoambiwa: Jilindeni kutokana na yaliyoko mbele yenu na yaliyoko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا تَأْتِيهِم مِّنْ ءَايَةٍ مِّنْ ءَايَٰتِ رَبِّهِمْ إِلَّا كَانُوا۟ عَنْهَا مُعْرِضِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi isipokuwa wao huwa ni wenye kuipa mgongo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ أَنفِقُوا۟ مِمَّا رَزَقَكُمُ ٱللَّهُ قَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لِلَّذِينَ ءَامَنُوٓا۟ أَنُطْعِمُ مَن لَّوْ يَشَآءُ ٱللَّهُ أَطْعَمَهُۥٓ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِى ضَلَٰلٍ مُّبِينٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wanapoambiwa: "Toeni katika aliyokupeni Mwenyezi Mungu", wale waliokufuru huwaambia wale walioamini: Je, tuwalishe wale ambao Mwenyezi Mungu angependa angeliwalisha mwenyewe? Nyinyi hammo isipokuwa katika upotovu ulio dhahiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا ٱلْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَٰدِقِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَا يَنظُرُونَ إِلَّا صَيْحَةً وَٰحِدَةً تَأْخُذُهُمْ وَهُمْ يَخِصِّمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hawangojei isipokuwa ukelele mmoja tu utakaowachukua nao wamo kuzozana.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَا يَسْتَطِيعُونَ تَوْصِيَةً وَلَآ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمْ يَرْجِعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنُفِخَ فِى ٱلصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ ٱلْأَجْدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يَنسِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na litapulizwa baragumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قَالُوا۟ يَٰوَيْلَنَا مَنۢ بَعَثَنَا مِن مَّرْقَدِنَا هَٰذَا مَا وَعَدَ ٱلرَّحْمَٰنُ وَصَدَقَ ٱلْمُرْسَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watasema: Ole wetu! Ni nani aliyetufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyoyaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَٰحِدَةً فَإِذَا هُمْ جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Haitakuwa isipokuwa ukelele mmoja tu, mara wote watahudhurishwa mbele yetu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَٱلْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْـًٔا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa isipokuwa yale mliyokuwa mkiyatenda.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ أَصْحَٰبَ ٱلْجَنَّةِ ٱلْيَوْمَ فِى شُغُلٍ فَٰكِهُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika watu wa Bustani ya mbinguni leo wamo shughulini, wamefurahi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
هُمْ وَأَزْوَٰجُهُمْ فِى ظِلَٰلٍ عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ مُتَّكِـُٔونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya kifahari.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَهُمْ فِيهَا فَٰكِهَةٌ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakachokitaka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سَلَٰمٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center "Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱمْتَٰزُوا۟ ٱلْيَوْمَ أَيُّهَا ٱلْمُجْرِمُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَلَمْ أَعْهَدْ إِلَيْكُمْ يَٰبَنِىٓ ءَادَمَ أَن لَّا تَعْبُدُوا۟ ٱلشَّيْطَٰنَ إِنَّهُۥ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, sikuagana nanyi, enyi wanadamu, kuwa msimuabudu Shetani? Hakika yeye ni adui dhahiri kwenu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَنِ ٱعْبُدُونِى هَٰذَا صِرَٰطٌ مُّسْتَقِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia iliyonyooka.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ أَضَلَّ مِنكُمْ جِبِلًّا كَثِيرًا أَفَلَمْ تَكُونُوا۟ تَعْقِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِى كُنتُمْ تُوعَدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hii basi ndiyo Jahannamu mliyokuwa mkiahidiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱصْلَوْهَا ٱلْيَوْمَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ingieni humo leo kwa vile mlivyokuwa mkikufuru.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَىٰٓ أَفْوَٰهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَآ أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyokuwa wakiyachuma.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَوْ نَشَآءُ لَطَمَسْنَا عَلَىٰٓ أَعْيُنِهِمْ فَٱسْتَبَقُوا۟ ٱلصِّرَٰطَ فَأَنَّىٰ يُبْصِرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tungelipenda, tungeliyafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wangeionaje?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَوْ نَشَآءُ لَمَسَخْنَٰهُمْ عَلَىٰ مَكَانَتِهِمْ فَمَا ٱسْتَطَٰعُوا۟ مُضِيًّا وَلَا يَرْجِعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tungelitaka, tungewageuza sura hapo hapo walipo, basi wasingeweza kwenda wala kurudi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَن نُّعَمِّرْهُ نُنَكِّسْهُ فِى ٱلْخَلْقِ أَفَلَا يَعْقِلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tunayemzeesha, tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je, hawazingatii?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا عَلَّمْنَٰهُ ٱلشِّعْرَ وَمَا يَنۢبَغِى لَهُۥٓ إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ وَقُرْءَانٌ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu isipokuwa ni ukumbusho na Qur-ani inayobainisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لِّيُنذِرَ مَن كَانَ حَيًّا وَيَحِقَّ ٱلْقَوْلُ عَلَى ٱلْكَٰفِرِينَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوَلَمْ يَرَوْا۟ أَنَّا خَلَقْنَا لَهُم مِّمَّا عَمِلَتْ أَيْدِينَآ أَنْعَٰمًا فَهُمْ لَهَا مَٰلِكُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyofanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَذَلَّلْنَٰهَا لَهُمْ فَمِنْهَا رَكُوبُهُمْ وَمِنْهَا يَأْكُلُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanaowapanda, na baadhi yao wanawala.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَهُمْ فِيهَا مَنَٰفِعُ وَمَشَارِبُ أَفَلَا يَشْكُرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱتَّخَذُوا۟ مِن دُونِ ٱللَّهِ ءَالِهَةً لَّعَلَّهُمْ يُنصَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَهُمْ وَهُمْ لَهُمْ جُندٌ مُّحْضَرُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio askari wao, watahudhurishwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَلَا يَحْزُنكَ قَوْلُهُمْ إِنَّا نَعْلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعْلِنُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayoyaweka siri na wanayoyadhihirisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوَلَمْ يَرَ ٱلْإِنسَٰنُ أَنَّا خَلَقْنَٰهُ مِن نُّطْفَةٍ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٌ مُّبِينٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwani mwanadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndiyo amekuwa ndiye mgomvi wa dhahiri!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَضَرَبَ لَنَا مَثَلًا وَنَسِىَ خَلْقَهُۥ قَالَ مَن يُحْىِ ٱلْعِظَٰمَ وَهِىَ رَمِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakayeihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قُلْ يُحْيِيهَا ٱلَّذِىٓ أَنشَأَهَآ أَوَّلَ مَرَّةٍ وَهُوَ بِكُلِّ خَلْقٍ عَلِيمٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Sema: Ataihuisha huyo huyo aliyeiumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلَّذِى جَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلشَّجَرِ ٱلْأَخْضَرِ نَارًا فَإِذَآ أَنتُم مِّنْهُ تُوقِدُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Aliyekujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَوَلَيْسَ ٱلَّذِى خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يَخْلُقَ مِثْلَهُم بَلَىٰ وَهُوَ ٱلْخَلَّٰقُ ٱلْعَلِيمُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwani aliyeziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi mno.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّمَآ أَمْرُهُۥٓ إِذَآ أَرَادَ شَيْـًٔا أَن يَقُولَ لَهُۥ كُن فَيَكُونُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika amri yake anapotaka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَسُبْحَٰنَ ٱلَّذِى بِيَدِهِۦ مَلَكُوتُ كُلِّ شَىْءٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
← Sura Faatir
Sura As-Saaffaat →
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
→
Matini ya Kiarabu na tafsiri kupitia Tanzil na QuranEnc — kama zilivyo, bila kubadilishwa · Tafsiri ni mali ya watafsiri wake na si Qur'ani yenyewe
Hii ni nyenzo ya utafiti, si chanzo cha fatwa.