caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Taa-Haa طه

Aya 135 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 45

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ طه

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTwa Ha![1]

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَآ أَنزَلْنَا عَلَيْكَ ٱلْقُرْءَانَ لِتَشْقَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHatukukuteremshia Qur-ani ili upate mashaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِلَّا تَذْكِرَةً لِّمَن يَخْشَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBali ni ukumbusho kwa mwenye kunyenyekea.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

تَنزِيلًا مِّمَّنْ خَلَقَ ٱلْأَرْضَ وَٱلسَّمَٰوَٰتِ ٱلْعُلَى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNi uteremsho kutoka kwa aliyeumba ardhi na mbingu zilizo juu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلرَّحْمَٰنُ عَلَى ٱلْعَرْشِ ٱسْتَوَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterArrahmani (Mwingi wa rehema), aliyeinuka juu ya Kiti cha Enzi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَهُۥ مَا فِى ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِى ٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَمَا تَحْتَ ٱلثَّرَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNi vyake vyote vilivyo katika mbingu na vilivyo katika ardhi, na vilivyo baina yake, na vilivyo chini ya ardhi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِن تَجْهَرْ بِٱلْقَوْلِ فَإِنَّهُۥ يَعْلَمُ ٱلسِّرَّ وَأَخْفَى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ukinyanyua sauti kwa kusema, basi hakika Yeye anajua siri na chini zaidi kuliko siri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ لَهُ ٱلْأَسْمَآءُ ٱلْحُسْنَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMwenyezi Mungu! Hakuna mungu yeyote isipokuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri zaidi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَهَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa je, imekufikia hadithi ya Musa?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذْ رَءَا نَارًا فَقَالَ لِأَهْلِهِ ٱمْكُثُوٓا۟ إِنِّىٓ ءَانَسْتُ نَارًا لَّعَلِّىٓ ءَاتِيكُم مِّنْهَا بِقَبَسٍ أَوْ أَجِدُ عَلَى ٱلنَّارِ هُدًى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAlipouona moto, kwa hivyo akawaambia ahali zake: Ngojeni! Hakika mimi nimeuona moto, huenda nikawaletea kijinga kutoka humo, au nikapata uongofu kwenye moto huo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلَمَّآ أَتَىٰهَا نُودِىَ يَٰمُوسَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi alipoufikia, akaitwa: Ewe Musa!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنِّىٓ أَنَا۠ رَبُّكَ فَٱخْلَعْ نَعْلَيْكَ إِنَّكَ بِٱلْوَادِ ٱلْمُقَدَّسِ طُوًى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani uko katika bonde takatifu la 'Tuwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَنَا ٱخْتَرْتُكَ فَٱسْتَمِعْ لِمَا يُوحَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNami nimekuteua wewe; basi sikiliza yanayofunuliwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّنِىٓ أَنَا ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱعْبُدْنِى وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ لِذِكْرِىٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hakuna mungu isipokuwa Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na udumishe Swala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱلسَّاعَةَ ءَاتِيَةٌ أَكَادُ أُخْفِيهَا لِتُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍۭ بِمَا تَسْعَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Saa itakuja bila ya shaka. Nimekaribia mno kuificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyoyafanya.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلَا يَصُدَّنَّكَ عَنْهَا مَن لَّا يُؤْمِنُ بِهَا وَٱتَّبَعَ هَوَىٰهُ فَتَرْدَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa hivyo, kamwe asikuzuilie nayo yule ambaye haiamini na akafuata matamanio yake ukaja kuangamia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَا تِلْكَ بِيَمِينِكَ يَٰمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ هِىَ عَصَاىَ أَتَوَكَّؤُا۟ عَلَيْهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِى وَلِىَ فِيهَا مَـَٔارِبُ أُخْرَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Hii ni fimbo yangu; ninaiegemea na ninawaangushia majani kwayo kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ أَلْقِهَا يَٰمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Itupe, ewe Musa!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَلْقَىٰهَا فَإِذَا هِىَ حَيَّةٌ تَسْعَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkaitupa. Mara ikawa nyoka anayekwenda mbio.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ خُذْهَا وَلَا تَخَفْ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا ٱلْأُولَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱضْمُمْ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخْرُجْ بَيْضَآءَ مِنْ غَيْرِ سُوٓءٍ ءَايَةً أُخْرَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa uambatishe mkono wako kwenye ubavu, utatoka mweupe pasipo na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyingine.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لِنُرِيَكَ مِنْ ءَايَٰتِنَا ٱلْكُبْرَى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIli tukuonyeshe katika ishara zetu kubwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNenda kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ رَبِّ ٱشْرَحْ لِى صَدْرِى

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Musa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيَسِّرْ لِىٓ أَمْرِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa nirahisishie kazi yangu hii.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱحْلُلْ عُقْدَةً مِّن لِّسَانِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa lifungue fundo lililo katika ulimi wangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَفْقَهُوا۟ قَوْلِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWapate kufahamu maneno yangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱجْعَل لِّى وَزِيرًا مِّنْ أَهْلِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa nipe msaidizi katika ahali zangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

هَٰرُونَ أَخِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHarun, kaka yangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱشْدُدْ بِهِۦٓ أَزْرِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwake yeye niongeze nguvu zangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَشْرِكْهُ فِىٓ أَمْرِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mshirikishe katika jambo langu hili.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَىْ نُسَبِّحَكَ كَثِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIli tukutakase kwa wingi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَنَذْكُرَكَ كَثِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tukutaje kwa wingi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّكَ كُنتَ بِنَا بَصِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Wewe unatuona vyema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ قَدْ أُوتِيتَ سُؤْلَكَ يَٰمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Hakika Umeshapewa maombi yako, ewe Musa!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَيْكَ مَرَّةً أُخْرَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika tulikwishakufanyia hisani mara nyingine.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذْ أَوْحَيْنَآ إِلَىٰٓ أُمِّكَ مَا يُوحَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterPale tulipomfunulia mama yako yaliyofunuliwa,

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَنِ ٱقْذِفِيهِ فِى ٱلتَّابُوتِ فَٱقْذِفِيهِ فِى ٱلْيَمِّ فَلْيُلْقِهِ ٱلْيَمُّ بِٱلسَّاحِلِ يَأْخُذْهُ عَدُوٌّ لِّى وَعَدُوٌّ لَّهُۥ وَأَلْقَيْتُ عَلَيْكَ مَحَبَّةً مِّنِّى وَلِتُصْنَعَ عَلَىٰ عَيْنِىٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterYa kuwa mtie katika kisanduku, na kisha kitie mtoni, na mto utamfikisha ufukweni. Atamchukua adui yangu naye ni adui yake. Na nimekutilia mapenzi yanayotoka kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذْ تَمْشِىٓ أُخْتُكَ فَتَقُولُ هَلْ أَدُلُّكُمْ عَلَىٰ مَن يَكْفُلُهُۥ فَرَجَعْنَٰكَ إِلَىٰٓ أُمِّكَ كَىْ تَقَرَّ عَيْنُهَا وَلَا تَحْزَنَ وَقَتَلْتَ نَفْسًا فَنَجَّيْنَٰكَ مِنَ ٱلْغَمِّ وَفَتَنَّٰكَ فُتُونًا فَلَبِثْتَ سِنِينَ فِىٓ أَهْلِ مَدْيَنَ ثُمَّ جِئْتَ عَلَىٰ قَدَرٍ يَٰمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterDada yako alipokwenda na akasema: Je! Niwajulishe mtu wa kuweza kumlea? Basi tukakurejesha kwa mama yako ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ulimuua mtu, nasi tukakuokoa katika dhiki, na tukakujaribu kwa majaribio mengi. Ukakaa miaka kwa watu wa Madyana. Kisha ukaja kama ilivyokadiriwa, ewe Musa!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱصْطَنَعْتُكَ لِنَفْسِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa nimekuteua kwa ajili ya nafsi yangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱذْهَبْ أَنتَ وَأَخُوكَ بِـَٔايَٰتِى وَلَا تَنِيَا فِى ذِكْرِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNenda, wewe na ndugu yako, pamoja na ishara zangu, wala msichoke kunikumbuka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱذْهَبَآ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَقُولَا لَهُۥ قَوْلًا لَّيِّنًا لَّعَلَّهُۥ يَتَذَكَّرُ أَوْ يَخْشَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَا رَبَّنَآ إِنَّنَا نَخَافُ أَن يَفْرُطَ عَلَيْنَآ أَوْ أَن يَطْغَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ لَا تَخَافَآ إِنَّنِى مَعَكُمَآ أَسْمَعُ وَأَرَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Msiogope! Hakika Mimi ni pamoja nanyi. Nasikia na ninaona.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأْتِيَاهُ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولَا رَبِّكَ فَأَرْسِلْ مَعَنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ وَلَا تُعَذِّبْهُمْ قَدْ جِئْنَٰكَ بِـَٔايَةٍ مِّن رَّبِّكَ وَٱلسَّلَٰمُ عَلَىٰ مَنِ ٱتَّبَعَ ٱلْهُدَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi mwendeeni, na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola wako Mlezi! Basi waache Wana wa Israili watoke nasi, wala usiwaadhibu. Sisi tumekuletea ishara itokayo kwa Mola wako Mlezi. Na amani iwe juu ya atakayefuata uongofu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّا قَدْ أُوحِىَ إِلَيْنَآ أَنَّ ٱلْعَذَابَ عَلَىٰ مَن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika tumefunuliwa sisi kwamba hakuna shaka adhabu itampata anayekadhibisha na akapuuza

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ فَمَن رَّبُّكُمَا يَٰمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Firauni) akasema: Basi Mola wenu Mlezi ni nani, ewe Musa?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ رَبُّنَا ٱلَّذِىٓ أَعْطَىٰ كُلَّ شَىْءٍ خَلْقَهُۥ ثُمَّ هَدَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Mola wetu Mlezi ni yule aliyekipa kila kitu umbo lake, kisha akakiongoa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ فَمَا بَالُ ٱلْقُرُونِ ٱلْأُولَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Nini hali ya karne za kwanza?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ عِلْمُهَا عِندَ رَبِّى فِى كِتَٰبٍ لَّا يَضِلُّ رَبِّى وَلَا يَنسَى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Elimu yake iko kwa Mola wangu Mlezi katika Kitabu. Mola wangu Mlezi hapotei wala hasahau.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِى جَعَلَ لَكُمُ ٱلْأَرْضَ مَهْدًا وَسَلَكَ لَكُمْ فِيهَا سُبُلًا وَأَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً فَأَخْرَجْنَا بِهِۦٓ أَزْوَٰجًا مِّن نَّبَاتٍ شَتَّىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbaye amewafanyia ardhi kuwa tandiko, na akawapitishia humo njia, na akawateremshia kutoka mbinguni maji. Na kwa hayo tukatoa namna mbalimbali za mimea.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كُلُوا۟ وَٱرْعَوْا۟ أَنْعَٰمَكُمْ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَٰتٍ لِّأُو۟لِى ٱلنُّهَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKuleni, na mchunge wanyama wenu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa wenye akili.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مِنْهَا خَلَقْنَٰكُمْ وَفِيهَا نُعِيدُكُمْ وَمِنْهَا نُخْرِجُكُمْ تَارَةً أُخْرَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTumewaumba kutokana nayo (ardhi), na humo tutawarudisha, na tutawatoa kutoka humo mara nyengine.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ أَرَيْنَٰهُ ءَايَٰتِنَا كُلَّهَا فَكَذَّبَ وَأَبَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika tulimwonyesha ishara zetu zote. Lakini alikadhibisha na akakataa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ أَجِئْتَنَا لِتُخْرِجَنَا مِنْ أَرْضِنَا بِسِحْرِكَ يَٰمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Ewe Musa! Hivyo umetujia kututoa katika nchi yetu kwa uchawi wako?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلَنَأْتِيَنَّكَ بِسِحْرٍ مِّثْلِهِۦ فَٱجْعَلْ بَيْنَنَا وَبَيْنَكَ مَوْعِدًا لَّا نُخْلِفُهُۥ نَحْنُ وَلَآ أَنتَ مَكَانًا سُوًى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi sisi hakika tutakuletea uchawi kama huo. Basi weka miadi baina yetu na wewe, ambayo tusiivunje sisi wala wewe, mahali patakapokuwa sawa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ مَوْعِدُكُمْ يَوْمُ ٱلزِّينَةِ وَأَن يُحْشَرَ ٱلنَّاسُ ضُحًى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Miadi yenu ni siku ya Sikukuu ya mapambo; na watu wakusanywe kabla ya adhuhuri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَتَوَلَّىٰ فِرْعَوْنُ فَجَمَعَ كَيْدَهُۥ ثُمَّ أَتَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi Firauni akageuka akarudi, na akatengeneza hila yake, kisha akaja.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ وَيْلَكُمْ لَا تَفْتَرُوا۟ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا فَيُسْحِتَكُم بِعَذَابٍ وَقَدْ خَابَ مَنِ ٱفْتَرَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMusa akawaambia: Ole wenu! Msimzulie Mwenyezi Mungu uongo, akaja kuwafutilia mbali kwa adhabu. Na hakika mwenye kuzua lazima ashindwe!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَتَنَٰزَعُوٓا۟ أَمْرَهُم بَيْنَهُمْ وَأَسَرُّوا۟ ٱلنَّجْوَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi wakazozana wenyewe kwa wenyewe kuhusiana na jambo lao hilo, na wakanong'ona kwa siri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوٓا۟ إِنْ هَٰذَٰنِ لَسَٰحِرَٰنِ يُرِيدَانِ أَن يُخْرِجَاكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِمَا وَيَذْهَبَا بِطَرِيقَتِكُمُ ٱلْمُثْلَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Hakika hawa wawili ni wachawi, wanataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wao, na waondoe mila zenu zilizo bora kabisa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَجْمِعُوا۟ كَيْدَكُمْ ثُمَّ ٱئْتُوا۟ صَفًّا وَقَدْ أَفْلَحَ ٱلْيَوْمَ مَنِ ٱسْتَعْلَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa hivyo kusanyeni hila zenu zote, kisha mfike kwa kujipanga safu, na kwa yakini atafuzu kweli kweli leo atakayeshinda.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ يَٰمُوسَىٰٓ إِمَّآ أَن تُلْقِىَ وَإِمَّآ أَن نَّكُونَ أَوَّلَ مَنْ أَلْقَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Ewe Musa! Ima utupe wewe, au tuwe sisi ndio wa kwanza wa kutupa?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ بَلْ أَلْقُوا۟ فَإِذَا حِبَالُهُمْ وَعِصِيُّهُمْ يُخَيَّلُ إِلَيْهِ مِن سِحْرِهِمْ أَنَّهَا تَسْعَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Bali tupeni nyinyi! Tahamaki! Kamba zao na fimbo zao zikaonekana mbele yake, kwa uchawi wao, kuwa zinakwenda mbio.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَوْجَسَ فِى نَفْسِهِۦ خِيفَةً مُّوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi Musa akaingia hofu katika nafsi yake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُلْنَا لَا تَخَفْ إِنَّكَ أَنتَ ٱلْأَعْلَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTukasema: Usihofu! Hakika wewe ndiye utakayeshinda.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَلْقِ مَا فِى يَمِينِكَ تَلْقَفْ مَا صَنَعُوٓا۟ إِنَّمَا صَنَعُوا۟ كَيْدُ سَٰحِرٍ وَلَا يُفْلِحُ ٱلسَّاحِرُ حَيْثُ أَتَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kitupe kilicho katika mkono wako wa kulia; kitavimeza walivyoviunda. Hakika walivyounda ni hila za mchawi tu, na mchawi hafanikiwi popote afikapo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأُلْقِىَ ٱلسَّحَرَةُ سُجَّدًا قَالُوٓا۟ ءَامَنَّا بِرَبِّ هَٰرُونَ وَمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi wachawi hao wakaangushwa chini wakasujudu. Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa Harun na Musa!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ ءَامَنتُمْ لَهُۥ قَبْلَ أَنْ ءَاذَنَ لَكُمْ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِى عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحْرَ فَلَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَٰفٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ فِى جُذُوعِ ٱلنَّخْلِ وَلَتَعْلَمُنَّ أَيُّنَآ أَشَدُّ عَذَابًا وَأَبْقَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Firauni) akasema: Oh! Mmemuamini kabla ya mimi kuwapa ruhusa? Hakika yeye ndiye mkubwa wenu aliyewafundisha uchawi huu. Basi kwa yakini nitawakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na lazima nitawatundika misalabani katika vigogo vya mitende, na hapo kwa yakini mtajua ni nani katika sisi ndiye mkali zaidi wa kuadhibu na kuiendeleza zaidi adhabu yake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ لَن نُّؤْثِرَكَ عَلَىٰ مَا جَآءَنَا مِنَ ٱلْبَيِّنَٰتِ وَٱلَّذِى فَطَرَنَا فَٱقْضِ مَآ أَنتَ قَاضٍ إِنَّمَا تَقْضِى هَٰذِهِ ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَآ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Hatutakupendelea wewe kuliko ishara waziwazi zilizotujia, na kuliko yule aliyetuumba. Basi hukumu utavyohukumu; kwani wewe hakika unahukumu tu haya ya maisha ya duniani.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّآ ءَامَنَّا بِرَبِّنَا لِيَغْفِرَ لَنَا خَطَٰيَٰنَا وَمَآ أَكْرَهْتَنَا عَلَيْهِ مِنَ ٱلسِّحْرِ وَٱللَّهُ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi uliotulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi (katika kuadhibu).

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّهُۥ مَن يَأْتِ رَبَّهُۥ مُجْرِمًا فَإِنَّ لَهُۥ جَهَنَّمَ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحْيَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika atakayemjia Mola wake Mlezi naye ni mhalifu, basi kwa yakini, yake huyo ni Jahannamu. Hafi humo wala haishi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَن يَأْتِهِۦ مُؤْمِنًا قَدْ عَمِلَ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَأُو۟لَٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلدَّرَجَٰتُ ٱلْعُلَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa anayemjia Yeye naye ni Muumini na akatenda mema, basi hao watakuwa na daraja za juu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

جَنَّٰتُ عَدْنٍ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا وَذَٰلِكَ جَزَآءُ مَن تَزَكَّىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBustani za milele zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Na hayo ndiyo malipo ya mwenye kujitakasa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ أَوْحَيْنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِى فَٱضْرِبْ لَهُمْ طَرِيقًا فِى ٱلْبَحْرِ يَبَسًا لَّا تَخَٰفُ دَرَكًا وَلَا تَخْشَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tulimfunulia Musa: Toka usiku na waja wangu, na uwapigie njia kavu baharini. Usihofu kukamatwa, wala usiogope.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَتْبَعَهُمْ فِرْعَوْنُ بِجُنُودِهِۦ فَغَشِيَهُم مِّنَ ٱلْيَمِّ مَا غَشِيَهُمْ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterFirauni akawafuata pamoja na majeshi yake. Basi kikawafudikiza humo baharini kilichowafudikiza.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَضَلَّ فِرْعَوْنُ قَوْمَهُۥ وَمَا هَدَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa Firauni aliwapoteza watu wake wala hakuwaongoa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَٰبَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ قَدْ أَنجَيْنَٰكُم مِّنْ عَدُوِّكُمْ وَوَٰعَدْنَٰكُمْ جَانِبَ ٱلطُّورِ ٱلْأَيْمَنَ وَنَزَّلْنَا عَلَيْكُمُ ٱلْمَنَّ وَٱلسَّلْوَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterEnyi Wana wa Israili! Hakika tuliwaokoa kutokana na adui yenu, na tukawaahidi upande wa kulia wa mlima na tukawateremshia Manna na Salwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كُلُوا۟ مِن طَيِّبَٰتِ مَا رَزَقْنَٰكُمْ وَلَا تَطْغَوْا۟ فِيهِ فَيَحِلَّ عَلَيْكُمْ غَضَبِى وَمَن يَحْلِلْ عَلَيْهِ غَضَبِى فَقَدْ هَوَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKuleni katika vitu vizuri hivyo tulivyowaruzuku, wala msiruke mipaka katika hayo, isije ikawashukia ghadhabu yangu. Na yule inayemshukia ghadhabu yangu basi huyo ameangamia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِنِّى لَغَفَّارٌ لِّمَن تَابَ وَءَامَنَ وَعَمِلَ صَٰلِحًا ثُمَّ ٱهْتَدَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika Mimi ni Mwingi wa kusamehe kwa anayetubia, na akaamini, na akatenda mema, kisha akaongoka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَآ أَعْجَلَكَ عَن قَوْمِكَ يَٰمُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa nini kilichokutia haraka ukawaacha watu wako, ewe Musa?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ هُمْ أُو۟لَآءِ عَلَىٰٓ أَثَرِى وَعَجِلْتُ إِلَيْكَ رَبِّ لِتَرْضَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Hao wapo nyuma yangu wananifuata. Na nimefanya haraka kukujia, Mola wangu Mlezi, ili uridhike.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ فَإِنَّا قَدْ فَتَنَّا قَوْمَكَ مِنۢ بَعْدِكَ وَأَضَلَّهُمُ ٱلسَّامِرِىُّ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Mwenyezi Mungu) akasema: Sisi tumewatia mtihani watu wako baada yako, na Msamaria amewapoteza.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَرَجَعَ مُوسَىٰٓ إِلَىٰ قَوْمِهِۦ غَضْبَٰنَ أَسِفًا قَالَ يَٰقَوْمِ أَلَمْ يَعِدْكُمْ رَبُّكُمْ وَعْدًا حَسَنًا أَفَطَالَ عَلَيْكُمُ ٱلْعَهْدُ أَمْ أَرَدتُّمْ أَن يَحِلَّ عَلَيْكُمْ غَضَبٌ مِّن رَّبِّكُمْ فَأَخْلَفْتُم مَّوْعِدِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi Musa akarudi kwa watu wake kwa ghadhabu na kusikitika. Akasema: Enyi watu wangu! Kwani Mola wenu Mlezi hakuwaahidi ahadi nzuri? Je, umekuwa muda mrefu kwenu au mmetaka ghadhabu ya Mola wenu Mlezi iwashukie, ndiyo maana mkavunja miadi yangu?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ مَآ أَخْلَفْنَا مَوْعِدَكَ بِمَلْكِنَا وَلَٰكِنَّا حُمِّلْنَآ أَوْزَارًا مِّن زِينَةِ ٱلْقَوْمِ فَقَذَفْنَٰهَا فَكَذَٰلِكَ أَلْقَى ٱلسَّامِرِىُّ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Sisi hatukuvunja miadi yako kwa hiari yetu, lakini tulibebeshwa mizigo ya mapambo ya watu, basi tukaitupa. Na hivyo ndivyo alivyotupa yule Msamaria.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَخْرَجَ لَهُمْ عِجْلًا جَسَدًا لَّهُۥ خُوَارٌ فَقَالُوا۟ هَٰذَآ إِلَٰهُكُمْ وَإِلَٰهُ مُوسَىٰ فَنَسِىَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa akawaundia ndama, kiwiliwili chenye sauti. Na wakasema: Huyu ndiye mungu wenu, na mungu wa Musa, lakini alisahau.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَفَلَا يَرَوْنَ أَلَّا يَرْجِعُ إِلَيْهِمْ قَوْلًا وَلَا يَمْلِكُ لَهُمْ ضَرًّا وَلَا نَفْعًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, hawakuona kuwa hakuwarudishia neno, wala kuwamilikia kudhuru wala kufaa?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ قَالَ لَهُمْ هَٰرُونُ مِن قَبْلُ يَٰقَوْمِ إِنَّمَا فُتِنتُم بِهِۦ وَإِنَّ رَبَّكُمُ ٱلرَّحْمَٰنُ فَٱتَّبِعُونِى وَأَطِيعُوٓا۟ أَمْرِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika Harun alikwishawaambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihanini tu kwa kitu hiki. Na kwa yakini Mola wenu Mlezi ni Arrahmani (Mwingi wa rehema). Basi nifuateni mimi, na tiini amri yangu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ لَن نَّبْرَحَ عَلَيْهِ عَٰكِفِينَ حَتَّىٰ يَرْجِعَ إِلَيْنَا مُوسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Hatutaacha kumwabudu mpaka Musa atakaporejea kwetu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ يَٰهَٰرُونُ مَا مَنَعَكَ إِذْ رَأَيْتَهُمْ ضَلُّوٓا۟

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Musa) akasema: Ewe Harun! Ni nini kilichokuzuia, ulipowaona wamepotea?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَلَّا تَتَّبِعَنِ أَفَعَصَيْتَ أَمْرِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUsinifuate. Je, umeasi amri yangu?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ يَبْنَؤُمَّ لَا تَأْخُذْ بِلِحْيَتِى وَلَا بِرَأْسِىٓ إِنِّى خَشِيتُ أَن تَقُولَ فَرَّقْتَ بَيْنَ بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ وَلَمْ تَرْقُبْ قَوْلِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Ewe mwana wa mama yangu! Usinishike ndevu zangu, wala kichwa changu. Kwa hakika naliogopa usijesema: Umewatenganisha Wana wa Israili, na hukungojea kauli yangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ فَمَا خَطْبُكَ يَٰسَٰمِرِىُّ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Musa) akasema: Ewe Msamaria! Unataka nini?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ بَصُرْتُ بِمَا لَمْ يَبْصُرُوا۟ بِهِۦ فَقَبَضْتُ قَبْضَةً مِّنْ أَثَرِ ٱلرَّسُولِ فَنَبَذْتُهَا وَكَذَٰلِكَ سَوَّلَتْ لِى نَفْسِى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Niliona wasiyoyaona wao, nikachukua mkamato wa mkono katika athari za unyayo wa Mtume. Kisha nikaitupa. Na hivi ndivyo ilivyonielekeza nafsi yangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ فَٱذْهَبْ فَإِنَّ لَكَ فِى ٱلْحَيَوٰةِ أَن تَقُولَ لَا مِسَاسَ وَإِنَّ لَكَ مَوْعِدًا لَّن تُخْلَفَهُۥ وَٱنظُرْ إِلَىٰٓ إِلَٰهِكَ ٱلَّذِى ظَلْتَ عَلَيْهِ عَاكِفًا لَّنُحَرِّقَنَّهُۥ ثُمَّ لَنَنسِفَنَّهُۥ فِى ٱلْيَمِّ نَسْفًا

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Musa) akasema: Basi ondoka! Na kwa yakini utakuwa katika maisha ukisema: Usiniguse. Na hakika una ahadi kwako isiyovunjwa. Na mtazame huyo mungu wako uliyeendelea kumuabudu. Sisi kwa hakika tutamchoma moto, kisha tutamtawanya sawasawa baharini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّمَآ إِلَٰهُكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِى لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ وَسِعَ كُلَّ شَىْءٍ عِلْمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika mungu wenu ni Allah (Mwenyezi Mungu) tu. Hakuna mungu isipokuwa Yeye. Amekienea kila kitu kwa elimu yake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَذَٰلِكَ نَقُصُّ عَلَيْكَ مِنْ أَنۢبَآءِ مَا قَدْ سَبَقَ وَقَدْ ءَاتَيْنَٰكَ مِن لَّدُنَّا ذِكْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNamna hivi tunakuhadithia katika khabari za yaliyotangulia. Na hakika tumekuletea kutoka kwetu mawaidha ya kukumbukwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَّنْ أَعْرَضَ عَنْهُ فَإِنَّهُۥ يَحْمِلُ يَوْمَ ٱلْقِيَٰمَةِ وِزْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAtakayeyapa mgongo, basi kwa yakini Siku ya Kiyama atabeba mzigo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

خَٰلِدِينَ فِيهِ وَسَآءَ لَهُمْ يَوْمَ ٱلْقِيَٰمَةِ حِمْلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWadumu humo. Na ni mzigo muovu kwao kuubeba Siku ya Kiyama!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ يُنفَخُ فِى ٱلصُّورِ وَنَحْشُرُ ٱلْمُجْرِمِينَ يَوْمَئِذٍ زُرْقًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku litakapopulizwa barugumu, na tukawakusanya wahalifu Siku hiyo, hali macho yao ni ya buluu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَتَخَٰفَتُونَ بَيْنَهُمْ إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا عَشْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatanong'onezana wao kwa wao: Hamkukaa ila siku kumi tu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

نَّحْنُ أَعْلَمُ بِمَا يَقُولُونَ إِذْ يَقُولُ أَمْثَلُهُمْ طَرِيقَةً إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا يَوْمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSisi tunajua zaidi watakayoyasema, atakaposema mbora wao katika mwendo: Nyinyi hamkukaa ila siku moja tu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيَسْـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلْجِبَالِ فَقُلْ يَنسِفُهَا رَبِّى نَسْفًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wanakuuliza habari za milima. Waambie: Mola wangu Mlezi ataivurugavuruga.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَيَذَرُهَا قَاعًا صَفْصَفًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ataiacha tambarare, uwanda.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَّا تَرَىٰ فِيهَا عِوَجًا وَلَآ أَمْتًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHutaona humo mdidimio wowote wala muinuko.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَئِذٍ يَتَّبِعُونَ ٱلدَّاعِىَ لَا عِوَجَ لَهُۥ وَخَشَعَتِ ٱلْأَصْوَاتُ لِلرَّحْمَٰنِ فَلَا تَسْمَعُ إِلَّا هَمْسًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku hiyo watamfuata muitaji huyo bila ya yeyote kumkengeuka. Na sauti zote zitamnyenyekea Arrahmani (Mwingi wa rehema). Basi hutasikia ila mnong'ono tu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَئِذٍ لَّا تَنفَعُ ٱلشَّفَٰعَةُ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحْمَٰنُ وَرَضِىَ لَهُۥ قَوْلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku hiyo uombezi hautafaa kitu, ila kwa atakayeruhusiwa na Arrahmani (Mwingi wa rehema) na akaridhia na maneno yake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يُحِيطُونَ بِهِۦ عِلْمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterYeye anajua yaliyo mbele yao, na yaliyo nyuma yao. Wala wao hawawezi kumjua Yeye vilivyo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَعَنَتِ ٱلْوُجُوهُ لِلْحَىِّ ٱلْقَيُّومِ وَقَدْ خَابَ مَنْ حَمَلَ ظُلْمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa zitadhalilika nyuso mbele ya Aliye Hai milele, Msimamia yote milele. Na atakuwa ameharibikiwa mwenye kubeba dhuluma.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَن يَعْمَلْ مِنَ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَا يَخَافُ ظُلْمًا وَلَا هَضْمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa anayetenda katika mema, naye ni Muumini, basi hatahofu kudhulumiwa wala kupunjwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَكَذَٰلِكَ أَنزَلْنَٰهُ قُرْءَانًا عَرَبِيًّا وَصَرَّفْنَا فِيهِ مِنَ ٱلْوَعِيدِ لَعَلَّهُمْ يَتَّقُونَ أَوْ يُحْدِثُ لَهُمْ ذِكْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa namna hivi tumeiteremsha Qur-ani kwa Kiarabu, na tumekariri humo vitisho ili wapate kuogopa na kujilinda na iwaletee makumbusho.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَتَعَٰلَى ٱللَّهُ ٱلْمَلِكُ ٱلْحَقُّ وَلَا تَعْجَلْ بِٱلْقُرْءَانِ مِن قَبْلِ أَن يُقْضَىٰٓ إِلَيْكَ وَحْيُهُۥ وَقُل رَّبِّ زِدْنِى عِلْمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki. Wala usiifanyie haraka hii Qur-ani, kabla haujamalizika ufunuo wake. Na sema: Mola wangu Mlezi! Nizidishie elimu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ عَهِدْنَآ إِلَىٰٓ ءَادَمَ مِن قَبْلُ فَنَسِىَ وَلَمْ نَجِدْ لَهُۥ عَزْمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hapo zamani tuliagana na Adam, lakini alisahau, wala hatukupata kwake azimio kubwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَٰٓئِكَةِ ٱسْجُدُوا۟ لِـَٔادَمَ فَسَجَدُوٓا۟ إِلَّآ إِبْلِيسَ أَبَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tulipowaambia Malaika: Msujudieni Adam! Wakasujudu, isipokuwa Iblisi, alikataa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَقُلْنَا يَٰٓـَٔادَمُ إِنَّ هَٰذَا عَدُوٌّ لَّكَ وَلِزَوْجِكَ فَلَا يُخْرِجَنَّكُمَا مِنَ ٱلْجَنَّةِ فَتَشْقَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTukasema: Ewe Adam! Hakika huyu ni adui yako na wa mkeo. Basi asiwatoe katika Bustani hii, mkaingia mashakani.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ لَكَ أَلَّا تَجُوعَ فِيهَا وَلَا تَعْرَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika humo hutakuwa na njaa wala hutakuwa uchi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَنَّكَ لَا تَظْمَؤُا۟ فِيهَا وَلَا تَضْحَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika hutapata kiu humo wala hutapata joto.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَوَسْوَسَ إِلَيْهِ ٱلشَّيْطَٰنُ قَالَ يَٰٓـَٔادَمُ هَلْ أَدُلُّكَ عَلَىٰ شَجَرَةِ ٱلْخُلْدِ وَمُلْكٍ لَّا يَبْلَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLakini Shetani alimtia wasiwasi, akamwambia: Ewe Adam! Nikujulishe mti wa kuishi maisha ya milele na ufalme usiokoma?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَكَلَا مِنْهَا فَبَدَتْ لَهُمَا سَوْءَٰتُهُمَا وَطَفِقَا يَخْصِفَانِ عَلَيْهِمَا مِن وَرَقِ ٱلْجَنَّةِ وَعَصَىٰٓ ءَادَمُ رَبَّهُۥ فَغَوَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi wakaula wote wawili, na uchi wao ukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani ya Bustanini. Na Adam akamuasi Mola wake Mlezi, na akapotea njia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ثُمَّ ٱجْتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَتَابَ عَلَيْهِ وَهَدَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKisha Mola wake Mlezi akamteua, na akamkubalia toba yake, na akamwongoa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ ٱهْبِطَا مِنْهَا جَمِيعًۢا بَعْضُكُمْ لِبَعْضٍ عَدُوٌّ فَإِمَّا يَأْتِيَنَّكُم مِّنِّى هُدًى فَمَنِ ٱتَّبَعَ هُدَاىَ فَلَا يَضِلُّ وَلَا يَشْقَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: Ondokeni humo nyote, hali ya kuwa ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Na ukiwafikia uongofu kutoka kwangu basi atakayeufuata uongofu wangu, hatapotea wala hatataabika.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَنْ أَعْرَضَ عَن ذِكْرِى فَإِنَّ لَهُۥ مَعِيشَةً ضَنكًا وَنَحْشُرُهُۥ يَوْمَ ٱلْقِيَٰمَةِ أَعْمَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa atakayeupa ukumbusho wangu mgongo, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa ni kipofu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ رَبِّ لِمَ حَشَرْتَنِىٓ أَعْمَىٰ وَقَدْ كُنتُ بَصِيرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAseme: Ewe Mola wangu Mlezi! Mbona umenifufua kipofu, nami nilikuwa nikiona vyema?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ كَذَٰلِكَ أَتَتْكَ ءَايَٰتُنَا فَنَسِيتَهَا وَكَذَٰلِكَ ٱلْيَوْمَ تُنسَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo hivyo. Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na vivyo hivyo leo utasahauliwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَكَذَٰلِكَ نَجْزِى مَنْ أَسْرَفَ وَلَمْ يُؤْمِنۢ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِۦ وَلَعَذَابُ ٱلْـَٔاخِرَةِ أَشَدُّ وَأَبْقَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hivyo ndivyo tutakavyomlipa kila apitaye kiasi, na asiziamini ishara za Mola wake Mlezi. Na hakika adhabu ya Akhera ni kali zaidi, na inadumu zaidi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَفَلَمْ يَهْدِ لَهُمْ كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّنَ ٱلْقُرُونِ يَمْشُونَ فِى مَسَٰكِنِهِمْ إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَـَٔايَٰتٍ لِّأُو۟لِى ٱلنُّهَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, haikuwabainikia ni ngapi katika vizazi tuliviangamiza kabla yao, nao wanatembea katika maskani zao? Hakika katika hayo zimo ishara kwa wenye akili.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَوْلَا كَلِمَةٌ سَبَقَتْ مِن رَّبِّكَ لَكَانَ لِزَامًا وَأَجَلٌ مُّسَمًّى

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa lau kuwa si neno lililokwishatangulia kutoka kwa Mola wako Mlezi na muda uliowekwa, bila ya shaka ingefika adhabu (duniani).

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ ٱلشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا وَمِنْ ءَانَآئِ ٱلَّيْلِ فَسَبِّحْ وَأَطْرَافَ ٱلنَّهَارِ لَعَلَّكَ تَرْضَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi yavumilie haya wayasemayo. Na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu kabla ya kuchomoza jua, na kabla ya kuzama kwake, na nyakati za usiku pia umtakase, na nyakati za mwisho za mchana ili upate ya kukuridhisha.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَا تَمُدَّنَّ عَيْنَيْكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعْنَا بِهِۦٓ أَزْوَٰجًا مِّنْهُمْ زَهْرَةَ ٱلْحَيَوٰةِ ٱلدُّنْيَا لِنَفْتِنَهُمْ فِيهِ وَرِزْقُ رَبِّكَ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWala kamwe usivikodolee macho tulivyowastarehesha kwavyo baadhi ya watu miongoni mwao, kwa ajili ya mapambo ya duniani, ili tuwajaribu katika hivyo. Na riziki ya Mola wako Mlezi ni bora na yenye kudumu zaidi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأْمُرْ أَهْلَكَ بِٱلصَّلَوٰةِ وَٱصْطَبِرْ عَلَيْهَا لَا نَسْـَٔلُكَ رِزْقًا نَّحْنُ نَرْزُقُكَ وَٱلْعَٰقِبَةُ لِلتَّقْوَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa waamrishe ahali zako kuswali, na usubiri juu yake. Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema ni kwa ucha Mungu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالُوا۟ لَوْلَا يَأْتِينَا بِـَٔايَةٍ مِّن رَّبِّهِۦٓ أَوَلَمْ تَأْتِهِم بَيِّنَةُ مَا فِى ٱلصُّحُفِ ٱلْأُولَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa walisema: "Kwa nini hakutuletea muujiza kutoka kwa Mola wake Mlezi?" Je, haukuwajia ushahidi wazi wa yaliyo katika Vitabu vya mwanzo?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَوْ أَنَّآ أَهْلَكْنَٰهُم بِعَذَابٍ مِّن قَبْلِهِۦ لَقَالُوا۟ رَبَّنَا لَوْلَآ أَرْسَلْتَ إِلَيْنَا رَسُولًا فَنَتَّبِعَ ءَايَٰتِكَ مِن قَبْلِ أَن نَّذِلَّ وَنَخْزَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa lau kuwa tuliwaangamiza kwa adhabu kabla yake, wangelisema: Ewe Mola wetu Mlezi! Kama ungetuletea Mtume (ingekuwa bora), tukazifuata ishara zako kabla ya kudhalilika na kuhizika.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُلْ كُلٌّ مُّتَرَبِّصٌ فَتَرَبَّصُوا۟ فَسَتَعْلَمُونَ مَنْ أَصْحَٰبُ ٱلصِّرَٰطِ ٱلسَّوِىِّ وَمَنِ ٱهْتَدَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSema: Kila mmoja anangoja. Basi ngojeni! Hivi karibuni mtajua ni akina nani ndio wenye njia sawa na ni nani aliyeongoka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70