Mwanzo › Sura › Sura Al-Qamar
Sura Al-Qamar القمر
Aya 55 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 37
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ ٱقْتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلْقَمَرُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَإِن يَرَوْا۟ ءَايَةً يُعْرِضُوا۟ وَيَقُولُوا۟ سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wakiona Ishara, hugeuka upande na husema: 'Huu uchawi tu unazidi kuendelea.'
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَكَذَّبُوا۟ وَٱتَّبَعُوٓا۟ أَهْوَآءَهُمْ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ جَآءَهُم مِّنَ ٱلْأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka zimewajia habari zenye makaripio.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
حِكْمَةٌۢ بَٰلِغَةٌ فَمَا تُغْنِ ٱلنُّذُرُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hekima kamili; lakini maonyo hayafai kitu!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ يَوْمَ يَدْعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَىْءٍ نُّكُرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi jiepushe nao. Siku atakapoita mwitaji kuliendea jambo linalochusha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
خُشَّعًا أَبْصَٰرُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige waliotawanyika.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مُّهْطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِ يَقُولُ ٱلْكَٰفِرُونَ هَٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: 'Hii ni siku ngumu.'
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا۟ عَبْدَنَا وَقَالُوا۟ مَجْنُونٌ وَٱزْدُجِرَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّى مَغْلُوبٌ فَٱنتَصِرْ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: 'Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!'
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَفَتَحْنَآ أَبْوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٍ مُّنْهَمِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayomiminika.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَفَجَّرْنَا ٱلْأَرْضَ عُيُونًا فَٱلْتَقَى ٱلْمَآءُ عَلَىٰٓ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukazipasua ardhi kwa chemichemi, yakakutana maji kwa jambo lililokwisha pangwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَحَمَلْنَٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَٰحٍ وَدُسُرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na tukambeba kwenye safina ya mbao na kamba.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
تَجْرِى بِأَعْيُنِنَا جَزَآءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ikawa inakwenda kwa macho yetu, kuwa ni malipo kwa aliyekuwa amekanushwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَد تَّرَكْنَٰهَآ ءَايَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anayekumbuka?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur-ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anayekumbuka?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kina 'Adi walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِى يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tuliwatumia upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilivyong'olewa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur-ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anayekumbuka?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَقَالُوٓا۟ أَبَشَرًا مِّنَّا وَٰحِدًا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذًا لَّفِى ضَلَٰلٍ وَسُعُرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wakasema: 'Ati tumfuate binadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotovu na kichaa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَءُلْقِىَ ٱلذِّكْرُ عَلَيْهِ مِنۢ بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ni yeye tu aliyeteremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mno, mshari mkubwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ ٱلْكَذَّابُ ٱلْأَشِرُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kesho watajua ni nani huyo mwongo mno, mshari mkubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا مُرْسِلُوا۟ ٱلنَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَٱرْتَقِبْهُمْ وَٱصْطَبِرْ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tutawatumia ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame vyema tu na ustahamili.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ ٱلْمَآءَ قِسْمَةٌۢ بَيْنَهُمْ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na waambie kwamba hakika maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliyehusika.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَنَادَوْا۟ صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَٰحِدَةً فَكَانُوا۟ كَهَشِيمِ ٱلْمُحْتَظِرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tuliwatumia ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea ua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur-ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍۭ بِٱلنُّذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ نَّجَّيْنَٰهُم بِسَحَرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika Sisi tukawatumia kimbunga cha vijiwe, isipokuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا كَذَٰلِكَ نَجْزِى مَن شَكَرَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa neema inayotoka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anayeshukuru.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا۟ بِٱلنُّذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِۦ فَطَمَسْنَآ أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: 'Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!'
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na hakika tumeisahilisha Qur-ani kuikumbuka. Lakini yupo anayekumbuka?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ جَآءَ ءَالَ فِرْعَوْنَ ٱلنُّذُرُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Waonyaji waliwajia watu wa Firauni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
كَذَّبُوا۟ بِـَٔايَٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَٰهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika mshiko wa Mwenye nguvu, Mwenye uwezo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُو۟لَٰٓئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَآءَةٌ فِى ٱلزُّبُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je, makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Au ndiyo wanasema: 'Sisi ni wengi tutashinda tu.'
Tazama tafsiri zote za aya hii →
سَيُهْزَمُ ٱلْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَٱلسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bali Saa ya Kiyama ndiyo miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ ٱلْمُجْرِمِينَ فِى ضَلَٰلٍ وَسُعُرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika wakosefu wamo katika upotovu na wazimu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِى ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا۟ مَسَّ سَقَرَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Siku watakapokokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: 'Onjeni mguso wa Saqar!'
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّا كُلَّ شَىْءٍ خَلَقْنَٰهُ بِقَدَرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَآ أَمْرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٌ كَلَمْحٍۭ بِٱلْبَصَرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَآ أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anayekumbuka?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَكُلُّ شَىْءٍ فَعَلُوهُ فِى ٱلزُّبُرِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kila jambo walilolifanya limo vitabuni.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍ وَنَهَرٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na mito.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فِى مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍۭ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Katika mahali pa kukalia pa haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
← Sura An-Najm
Sura Ar-Rahmaan →
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
→
Matini ya Kiarabu na tafsiri kupitia Tanzil na QuranEnc — kama zilivyo, bila kubadilishwa · Tafsiri ni mali ya watafsiri wake na si Qur'ani yenyewe
Hii ni nyenzo ya utafiti, si chanzo cha fatwa.