caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura At-Tur الطور

Aya 49 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 76

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلطُّورِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNinaapa kwa mlima wa T'ur.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَكِتَٰبٍ مَّسْطُورٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa Kitabu kilichoandikwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فِى رَقٍّ مَّنشُورٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKatika ngozi iliyokunjuliwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلْبَيْتِ ٱلْمَعْمُورِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa Nyumba iliyojengwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلسَّقْفِ ٱلْمَرْفُوعِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa dari iliyonyanyuliwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلْبَحْرِ ٱلْمَسْجُورِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa bahari iliyojazwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHapana wa kuizuia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku zitakapotikisika mbingu kwa mtikiso.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَتَسِيرُ ٱلْجِبَالُ سَيْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَوَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi ole wao siku hiyo hao wanaokadhibisha.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِينَ هُمْ فِى خَوْضٍ يَلْعَبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbao wanacheza katika mambo ya upuuzi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku watakaposukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِى كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mliokuwa mkiukadhibisha!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَفَسِحْرٌ هَٰذَآ أَمْ أَنتُمْ لَا تُبْصِرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, huu ni uchawi, au hamwoni tu?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱصْلَوْهَا فَٱصْبِرُوٓا۟ أَوْ لَا تَصْبِرُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْكُمْ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyokuwa mkiyatenda.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍ وَنَعِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani na neema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَىٰهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ ٱلْجَحِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakifurahi kwa yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda kutokana na adhabu ya Motoni.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyokuwa mkiyatenda.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٍ مَّصْفُوفَةٍ وَزَوَّجْنَٰهُم بِحُورٍ عِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyopangwa kwa safu. Na tutawaoza mahurulaini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَٱتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَآ أَلَتْنَٰهُم مِّنْ عَمَلِهِم مِّن شَىْءٍ كُلُّ ٱمْرِئٍۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wale walioamini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani, tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alichokichuma.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَمْدَدْنَٰهُم بِفَٰكِهَةٍ وَلَحْمٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tutawapa matunda, na nyama kama watakavyopenda.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأْسًا لَّا لَغْوٌ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatapeana humo bilauri zisizo na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌ لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌ مَّكْنُونٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWataelekeana wakiulizana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوٓا۟ إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِىٓ أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWaseme: Hakika tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa mno.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيْنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda mbali adhabu ya upepo wa Moto.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwingi wa kurehemu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَذَكِّرْ فَمَآ أَنتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍ وَلَا مَجْنُونٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيْبَ ٱلْمَنُونِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُلْ تَرَبَّصُوا۟ فَإِنِّى مَعَكُم مِّنَ ٱلْمُتَرَبِّصِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلَٰمُهُم بِهَٰذَآ أَمْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥ بَل لَّا يُؤْمِنُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu ndiyo wanasema: 'Ameitunga hii!' Bali basi tu hawaamini!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلْيَأْتُوا۟ بِحَدِيثٍ مِّثْلِهِۦٓ إِن كَانُوا۟ صَٰدِقِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ خُلِقُوا۟ مِنْ غَيْرِ شَىْءٍ أَمْ هُمُ ٱلْخَٰلِقُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ خَلَقُوا۟ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ بَل لَّا يُوقِنُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ عِندَهُمْ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ ٱلْمُصَۣيْطِرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wanazo hazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ لَهُمْ سُلَّمٌ يَسْتَمِعُونَ فِيهِ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُم بِسُلْطَٰنٍ مُّبِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja iliyo wazi!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ لَهُ ٱلْبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلْبَنُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wanayo elimu ya ghaibu, nao wameandika?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدًا فَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ هُمُ ٱلْمَكِيدُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao waliokufuru ndio watakaotegeka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ لَهُمْ إِلَٰهٌ غَيْرُ ٱللَّهِ سُبْحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wanaye mungu asiyekuwa Mwenyezi Mungu? Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hao wanaowashirikisha naye.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِن يَرَوْا۟ كِسْفًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطًا يَقُولُوا۟ سَحَابٌ مَّرْكُومٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hata wangeona pande linatoka mbinguni linaanguka wangesema: Ni mawingu yaliyobebana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَذَرْهُمْ حَتَّىٰ يُلَٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى فِيهِ يُصْعَقُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi waache mpaka wakutane na siku yao watakapohilikishwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ لَا يُغْنِى عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْـًٔا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ عَذَابًا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hii, lakini wengi wao hawajui.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمِنَ ٱلَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَٰرَ ٱلنُّجُومِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa usiku pia mtakase, na zinapokuchwa nyota.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70