caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Adh-Dhaariyat الذاريات

Aya 60 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 67

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلذَّٰرِيَٰتِ ذَرْوًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNinaapa kwa pepo zinazotawanya.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱلْحَٰمِلَٰتِ وِقْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa zinazobeba mizigo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱلْجَٰرِيَٰتِ يُسْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa zinazokwenda kwa wepesi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱلْمُقَسِّمَٰتِ أَمْرًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa zinazogawanya kwa amri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika mnayoahidiwa bila ya shaka ni ya ukweli.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْحُبُكِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNinaapa kwa mbingu zenye njia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّكُمْ لَفِى قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayohitalifiana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAnageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قُتِلَ ٱلْخَرَّٰصُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWazushi wameangamizwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِينَ هُمْ فِى غَمْرَةٍ سَاهُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbao wameghafilika katika ujinga.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَسْـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ ٱلدِّينِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWanauliza: 'Ni lini hiyo siku ya malipo?'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ هُمْ عَلَى ٱلنَّارِ يُفْتَنُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHiyo ni siku watakayoadhibiwa Motoni.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ذُوقُوا۟ فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تَسْتَعْجِلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterOnjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyokuwa mkiyafanyia haraka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika wacha Mungu watakuwa katika Mabustani ya mbinguni na chemchemi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ءَاخِذِينَ مَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWanapokea yale aliyowapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَانُوا۟ قَلِيلًا مِّنَ ٱلَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWalikuwa wakilala kidogo tu usiku.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَبِٱلْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiyeomba.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفِى ٱلْأَرْضِ ءَايَٰتٌ لِّلْمُوقِنِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفِىٓ أَنفُسِكُمْ أَفَلَا تُبْصِرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa pia katika nafsi zenu - Je, hamwoni?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفِى ٱلسَّمَآءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika mbingu ziko riziki zenu na yale mnayoahidiwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَوَرَبِّ ٱلسَّمَآءِ وَٱلْأَرْضِ إِنَّهُۥ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَآ أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi ninaapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَٰهِيمَ ٱلْمُكْرَمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanaoheshimiwa?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذْ دَخَلُوا۟ عَلَيْهِ فَقَالُوا۟ سَلَٰمًا قَالَ سَلَٰمٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWalipoingia kwake na wakasema: 'Salama!' Na yeye akasema: 'Salama! Nyinyi ni watu nisiowajua.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهْلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi akaenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliyenona.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkawakaribishia, akasema: 'Mbona hamli?'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً قَالُوا۟ لَا تَخَفْ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa hivyo, akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: 'Usiwe na hofu.' Basi wakambashiria kupata kijana mwenye elimu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَقْبَلَتِ ٱمْرَأَتُهُۥ فِى صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNdipo mkewe akawaelekea kwa sauti ya kelele huku anajipiga usoni kwa mastaajabu, akasema: "Mimi ni kikongwe na tasa!"

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْحَكِيمُ ٱلْعَلِيمُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyosema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا ٱلْمُرْسَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: 'Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mliotumwa?'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوٓا۟ إِنَّآ أُرْسِلْنَآ إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: 'Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTuwatupie mawe ya udongo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterYaliyotiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanaopindukia mipaka.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa hivyo tukawatoa katika hao wale walioamini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ ٱلْمُسْلِمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَتَرَكْنَا فِيهَآ ءَايَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ ٱلْعَذَابَ ٱلْأَلِيمَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanaoiogopa adhabu chungu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفِى مُوسَىٰٓ إِذْ أَرْسَلْنَٰهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَٰنٍ مُّبِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika habari za Musa, tulipomtuma kwa Firauni na hoja wazi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِۦ وَقَالَ سَٰحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu!'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَخَذْنَٰهُ وَجُنُودَهُۥ فَنَبَذْنَٰهُمْ فِى ٱلْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, huku ni wa kulaumiwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفِى عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ ٱلرِّيحَ ٱلْعَقِيمَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika habari za 'Adi tulipowatumia upepo wa kukata uzazi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَا تَذَرُ مِن شَىْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَٱلرَّمِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHaukuacha chochote ulichokifikia ila ulikifanya kama kilichonyambuka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفِى ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا۟ حَتَّىٰ حِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika habari za Thamudi walipoambiwa: 'Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَعَتَوْا۟ عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ ٱلصَّٰعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi ukawanyakua moto wa radi nao wanaona.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَمَا ٱسْتَطَٰعُوا۟ مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا۟ مُنتَصِرِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ قَوْمًا فَٰسِقِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلسَّمَآءَ بَنَيْنَٰهَا بِأَيْي۟دٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio wenye uwezo wa kuzitanua.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلْأَرْضَ فَرَشْنَٰهَا فَنِعْمَ ٱلْمَٰهِدُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمِن كُلِّ شَىْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَفِرُّوٓا۟ إِلَى ٱللَّهِ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَا تَجْعَلُوا۟ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ إِنِّى لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَذَٰلِكَ مَآ أَتَى ٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا۟ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: 'Huyu ni mchawi au mwendawazimu.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَتَوَاصَوْا۟ بِهِۦ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَآ أَنتَ بِمَلُومٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَذَكِّرْ فَإِنَّ ٱلذِّكْرَىٰ تَنفَعُ ٱلْمُؤْمِنِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَا خَلَقْتُ ٱلْجِنَّ وَٱلْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَآ أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَآ أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلرَّزَّاقُ ذُو ٱلْقُوَّةِ ٱلْمَتِينُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَٰبِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika wale waliodhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasiniharakishe.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا۟ مِن يَوْمِهِمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi ole wao wale walioikanusha siku yao waliyoahidiwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70