caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Al-Qalam القلم

Aya 52 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 2

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ نٓ وَٱلْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.[1]

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَآ أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika wewe una tabia tukufu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKaribu utaona, na wao wataona.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

بِأَييِّكُمُ ٱلْمَفْتُونُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNi nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعْلَمُ بِٱلْمُهْتَدِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Mola wako Mlezi ndiye ajuaye zaidi ni nani aliyeipotea njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلَا تُطِعِ ٱلْمُكَذِّبِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi usiwatii wanaokadhibisha.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَدُّوا۟ لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWalitamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWala usimtii kila mwingi wa kuapa, anayedharauliwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

هَمَّازٍ مَّشَّآءٍۭ بِنَمِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMwenye kukejeli mno, anayetangatanga akieneza maneno ya kufitini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

عُتُلٍّۭ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMkatili, na juu ya hayo, ni mshari aliyejipachika tu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAti kwa kuwa ana mali na watoto!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAnaposomewa Aya zetu, husema: "(Hizi ni) simulizi za uongo za watu wa zamani!"

Tazama tafsiri zote za aya hii →

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلْخُرْطُومِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterTutamtia alama kwenye pua yake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّا بَلَوْنَٰهُمْ كَمَا بَلَوْنَآ أَصْحَٰبَ ٱلْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا۟ لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika tuliwajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba lazima watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَا يَسْتَثْنُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWala hawakusema: "Mwenyezi Mungu akipenda!"

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَطَافَ عَلَيْهَا طَآئِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَآئِمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَصْبَحَتْ كَٱلصَّرِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLikawa kama usiku wa giza.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَتَنَادَوْا۟ مُصْبِحِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKisha asubuhi wakaitana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَنِ ٱغْدُوا۟ عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَٰرِمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterYa kwamba: "Nendeni mapema kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna."

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱنطَلَقُوا۟ وَهُمْ يَتَخَٰفَتُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi walikwenda huku wananong'onezana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا ٱلْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterYa kuwa: "Leo kamwe masikini mmoja asikuingilieni."

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَغَدَوْا۟ عَلَىٰ حَرْدٍ قَٰدِرِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوٓا۟ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBali tumenyimwa!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ سُبْحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَٰوَمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi wakaelekeana kulaumiana wao kwa wao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالُوا۟ يَٰوَيْلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakasema: Ole wetu! Hakika sisi tulikuwa tumeikiuka mipaka!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAsaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَذَٰلِكَ ٱلْعَذَابُ وَلَعَذَابُ ٱلْـَٔاخِرَةِ أَكْبَرُ لَوْ كَانُوا۟ يَعْلَمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNamna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangelijua!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَفَنَجْعَلُ ٱلْمُسْلِمِينَ كَٱلْمُجْرِمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwani tutawafanya Waislamu kama wahalifu?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMna nini? Mnahukumu vipi?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ لَكُمْ كِتَٰبٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKuwa mtapata humo mnayoyapenda?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ لَكُمْ أَيْمَٰنٌ عَلَيْنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ ٱلْقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWaulize: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa haya?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ لَهُمْ شُرَكَآءُ فَلْيَأْتُوا۟ بِشُرَكَآئِهِمْ إِن كَانُوا۟ صَٰدِقِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza

Tazama tafsiri zote za aya hii →

خَٰشِعَةً أَبْصَٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ وَقَدْ كَانُوا۟ يُدْعَوْنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمْ سَٰلِمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMacho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa wazima.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَذَرْنِى وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلْحَدِيثِ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi niache na wanaokadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kutokea mahali wasipopajua.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأُمْلِى لَهُمْ إِنَّ كَيْدِى مَتِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAu iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, aliponadi naye kazongwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَّوْلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلْعَرَآءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angelitupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱجْتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَٰرِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا۟ ٱلذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجْنُونٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَٰلَمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70