caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Qaaf ق

Aya 45 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 34

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ قٓ وَٱلْقُرْءَانِ ٱلْمَجِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterQaaf.[1] Ninaapa kwa Qur-ani tukufu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

بَلْ عَجِبُوٓا۟ أَن جَآءَهُم مُّنذِرٌ مِّنْهُمْ فَقَالَ ٱلْكَٰفِرُونَ هَٰذَا شَىْءٌ عَجِيبٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: 'Hili ni jambo la ajabu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَءِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا ذَٰلِكَ رَجْعٌۢ بَعِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAti tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَدْ عَلِمْنَا مَا تَنقُصُ ٱلْأَرْضُ مِنْهُمْ وَعِندَنَا كِتَٰبٌ حَفِيظٌۢ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinachopunguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinachohifadhi vyema yote.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

بَلْ كَذَّبُوا۟ بِٱلْحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمْ فَهُمْ فِىٓ أَمْرٍ مَّرِيجٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLakini waliikanusha Haki ilipowajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mchanganyiko.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَفَلَمْ يَنظُرُوٓا۟ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَوْقَهُمْ كَيْفَ بَنَيْنَٰهَا وَزَيَّنَّٰهَا وَمَا لَهَا مِن فُرُوجٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyozijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلْأَرْضَ مَدَدْنَٰهَا وَأَلْقَيْنَا فِيهَا رَوَٰسِىَ وَأَنۢبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍۭ بَهِيجٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

تَبْصِرَةً وَذِكْرَىٰ لِكُلِّ عَبْدٍ مُّنِيبٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterYawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kurejea (kwa Mwenyezi Mungu).

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَنَزَّلْنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءً مُّبَٰرَكًا فَأَنۢبَتْنَا بِهِۦ جَنَّٰتٍ وَحَبَّ ٱلْحَصِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyobarikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلنَّخْلَ بَاسِقَٰتٍ لَّهَا طَلْعٌ نَّضِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mitende mirefu yenye makole yaliyozaa kwa wingi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

رِّزْقًا لِّلْعِبَادِ وَأَحْيَيْنَا بِهِۦ بَلْدَةً مَّيْتًا كَذَٰلِكَ ٱلْخُرُوجُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIli iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyokuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyokuwa ufufuaji.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَأَصْحَٰبُ ٱلرَّسِّ وَثَمُودُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakazi wa Rassi na Thamudi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَعَادٌ وَفِرْعَوْنُ وَإِخْوَٰنُ لُوطٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa A'di na Firauni na kaumu ya Luti.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَصْحَٰبُ ٱلْأَيْكَةِ وَقَوْمُ تُبَّعٍ كُلٌّ كَذَّبَ ٱلرُّسُلَ فَحَقَّ وَعِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wakazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَفَعَيِينَا بِٱلْخَلْقِ ٱلْأَوَّلِ بَلْ هُمْ فِى لَبْسٍ مِّنْ خَلْقٍ جَدِيدٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza? Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ خَلَقْنَا ٱلْإِنسَٰنَ وَنَعْلَمُ مَا تُوَسْوِسُ بِهِۦ نَفْسُهُۥ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْ حَبْلِ ٱلْوَرِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika tulimuumba mtu, nasi tunayajua yanayomtia wasiwasi katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذْ يَتَلَقَّى ٱلْمُتَلَقِّيَانِ عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ قَعِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWanapopokea wapokeaji wawili, wanaokaa kuliani na kushotoni.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَجَآءَتْ سَكْرَةُ ٱلْمَوْتِ بِٱلْحَقِّ ذَٰلِكَ مَا كُنتَ مِنْهُ تَحِيدُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyokuwa ukiyakimbia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَنُفِخَ فِى ٱلصُّورِ ذَٰلِكَ يَوْمُ ٱلْوَعِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَجَآءَتْ كُلُّ نَفْسٍ مَّعَهَا سَآئِقٌ وَشَهِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَّقَدْ كُنتَ فِى غَفْلَةٍ مِّنْ هَٰذَا فَكَشَفْنَا عَنكَ غِطَآءَكَ فَبَصَرُكَ ٱلْيَوْمَ حَدِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Aambiwe): 'Kwa hakika ulikuwa umeghafilika mbali na haya. Basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali mno.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَقَالَ قَرِينُهُۥ هَٰذَا مَا لَدَىَّ عَتِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mwenzake atasema: 'Huyu niliye naye mimi keshatayarishwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَلْقِيَا فِى جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMtupeni katika Jahanamu kila kafiri mkubwa mkaidi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ مُّرِيبٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkatazaye mno heri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِى جَعَلَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَأَلْقِيَاهُ فِى ٱلْعَذَابِ ٱلشَّدِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAliyeweka mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ قَرِينُهُۥ رَبَّنَا مَآ أَطْغَيْتُهُۥ وَلَٰكِن كَانَ فِى ضَلَٰلٍۭ بَعِيدٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMwenzake aseme: 'Ewe Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

قَالَ لَا تَخْتَصِمُوا۟ لَدَىَّ وَقَدْ قَدَّمْتُ إِلَيْكُم بِٱلْوَعِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Mwenyezi Mungu) aseme: 'Msigombane mbele yangu. Tayari niliwaletea mbele onyo langu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَا يُبَدَّلُ ٱلْقَوْلُ لَدَىَّ وَمَآ أَنَا۠ بِظَلَّٰمٍ لِّلْعَبِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ ٱمْتَلَأْتِ وَتَقُولُ هَلْ مِن مَّزِيدٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku tutakapoiambia Jahanamu: 'Je, umejaa?' Nayo itasema: 'Je, kuna ziada?'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأُزْلِفَتِ ٱلْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ غَيْرَ بَعِيدٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa Bustani ya mbinguni italetwa karibu mno kwa ajili ya wacha Mungu, haitakuwa mbali.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِكُلِّ أَوَّابٍ حَفِيظٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHaya ndiyo mnayoahidiwa kwa kila mwenye kurejea mno kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda vyema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَّنْ خَشِىَ ٱلرَّحْمَٰنَ بِٱلْغَيْبِ وَجَآءَ بِقَلْبٍ مُّنِيبٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMwenye kumwogopa mno Mwingi wa rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo uliotubia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱدْخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ذَٰلِكَ يَوْمُ ٱلْخُلُودِ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Ataambiwa) ingieni humo kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya kudumu daima dawamu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَهُم مَّا يَشَآءُونَ فِيهَا وَلَدَيْنَا مَزِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHumo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَكَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّن قَرْنٍ هُمْ أَشَدُّ مِنْهُم بَطْشًا فَنَقَّبُوا۟ فِى ٱلْبِلَٰدِ هَلْ مِن مَّحِيصٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao, waliokuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je, walipata pa kukimbilia?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ فِى ذَٰلِكَ لَذِكْرَىٰ لِمَن كَانَ لَهُۥ قَلْبٌ أَوْ أَلْقَى ٱلسَّمْعَ وَهُوَ شَهِيدٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ خَلَقْنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِى سِتَّةِ أَيَّامٍ وَمَا مَسَّنَا مِن لُّغُوبٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake katika siku sita; na wala hayakutugusa machovu yoyote.[1]

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ ٱلشَّمْسِ وَقَبْلَ ٱلْغُرُوبِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمِنَ ٱلَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَأَدْبَٰرَ ٱلسُّجُودِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱسْتَمِعْ يَوْمَ يُنَادِ ٱلْمُنَادِ مِن مَّكَانٍ قَرِيبٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa sikiliza siku atakaponadi mwenye kunadi kutoka mahali karibu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ يَسْمَعُونَ ٱلصَّيْحَةَ بِٱلْحَقِّ ذَٰلِكَ يَوْمُ ٱلْخُرُوجِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku watakaposikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّا نَحْنُ نُحْىِۦ وَنُمِيتُ وَإِلَيْنَا ٱلْمَصِيرُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ تَشَقَّقُ ٱلْأَرْضُ عَنْهُمْ سِرَاعًا ذَٰلِكَ حَشْرٌ عَلَيْنَا يَسِيرٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku itapowapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

نَّحْنُ أَعْلَمُ بِمَا يَقُولُونَ وَمَآ أَنتَ عَلَيْهِم بِجَبَّارٍ فَذَكِّرْ بِٱلْقُرْءَانِ مَن يَخَافُ وَعِيدِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur-ani anayeliogopa onyo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70