caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Al-Mutaffifin المطففين

Aya 36 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 86

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterOle wao hao wapunjao!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكْتَالُوا۟ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسْتَوْفُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbao wanapojipimia kwa watu hudai watimiziwe.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wao wanapowapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَلَا يَظُنُّ أُو۟لَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لِيَوْمٍ عَظِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKatika Siku iliyo kuu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلْعَٰلَمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku watakapomsimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْفُجَّارِ لَفِى سِجِّينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا سِجِّينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUnajua nini Sijjin?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كِتَٰبٌ مَّرْقُومٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKitabu kilichoandikwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterOle wao siku hiyo kwa wanaokadhibisha!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلْأَوَّلِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAnaposomewa Aya zetu husema: "Ni visa vya watu wa kale!"

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَلَّا بَلْ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا۟ يَكْسِبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao waliokuwa wakiyachuma.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَلَّآ إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa mbali na neema za Mola wao Mlezi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُوا۟ ٱلْجَحِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKisha wataingia Motoni!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِى كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKisha waambiwe: Haya ndiyo mliyokuwa mkiyakadhibisha.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلْأَبْرَارِ لَفِى عِلِّيِّينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika Illiyyin.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa nini kitakachokujuvya nini Iliyyin?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كِتَٰبٌ مَّرْقُومٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKitabu kilichoandikwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَشْهَدُهُ ٱلْمُقَرَّبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWanakishuhudia waliokaribishwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱلْأَبْرَارَ لَفِى نَعِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

تَعْرِفُ فِى وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ ٱلنَّعِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUtatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatanyweshwa kinywaji safi kilichozibwa vyema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

خِتَٰمُهُۥ مِسْكٌ وَفِى ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ ٱلْمُتَنَٰفِسُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKizibo chake ni miski. Na katika hayo na washindanie wenye kushindana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسْنِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mchanganyiko wake ni Tasniim.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا ٱلْمُقَرَّبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterChemchemi watakayoinywa waliokurubishwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجْرَمُوا۟ كَانُوا۟ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ يَضْحَكُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa hakika wale waliokuwa wahalifu walikuwa wakiwacheka walioamini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَا مَرُّوا۟ بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wanapopita karibu yao wakikonyezana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓا۟ إِلَىٰٓ أَهْلِهِمُ ٱنقَلَبُوا۟ فَكِهِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wanaporudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوٓا۟ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wanapowaona husema: Hakika hawa ndio hasa waliopotea.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَآ أُرْسِلُوا۟ عَلَيْهِمْ حَٰفِظِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱلْيَوْمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ مِنَ ٱلْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi leo walioamini ndio watawacheka makafiri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

عَلَى ٱلْأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

هَلْ ثُوِّبَ ٱلْكُفَّارُ مَا كَانُوا۟ يَفْعَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70