caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Ad-Dukhaan الدخان

Aya 59 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 64

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ حمٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHa Mim.[1]

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلْكِتَٰبِ ٱلْمُبِينِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNinaapa kwa Kitabu kinachobainisha.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّآ أَنزَلْنَٰهُ فِى لَيْلَةٍ مُّبَٰرَكَةٍ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Sisi tumekiteremsha katika usiku uliobarikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKatika usiku huu hubainishwa kila jambo la hekima.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَمْرًا مِّنْ عِندِنَآ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلْعَلِيمُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNi rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

رَبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَآ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْىِۦ وَيُمِيتُ رَبُّكُمْ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلْأَوَّلِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

بَلْ هُمْ فِى شَكٍّ يَلْعَبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLakini wao wanacheza katika shaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱرْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِى ٱلسَّمَآءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi ingoje siku ambayo mbingu zitakapoleta moshi ulio dhahiri.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَغْشَى ٱلنَّاسَ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUtakaowafunika watu. Hii ni adhabu chungu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

رَّبَّنَا ٱكْشِفْ عَنَّا ٱلْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَنَّىٰ لَهُمُ ٱلذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَآءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ثُمَّ تَوَلَّوْا۟ عَنْهُ وَقَالُوا۟ مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wao wakamgeuzia uso, na wakasema: 'Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّا كَاشِفُوا۟ ٱلْعَذَابِ قَلِيلًا إِنَّكُمْ عَآئِدُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ نَبْطِشُ ٱلْبَطْشَةَ ٱلْكُبْرَىٰٓ إِنَّا مُنتَقِمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku tutakayoyashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَآءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَنْ أَدُّوٓا۟ إِلَىَّ عِبَادَ ٱللَّهِ إِنِّى لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkasema: 'Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَأَن لَّا تَعْلُوا۟ عَلَى ٱللَّهِ إِنِّىٓ ءَاتِيكُم بِسُلْطَٰنٍ مُّبِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِنِّى عُذْتُ بِرَبِّى وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا۟ لِى فَٱعْتَزِلُونِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَٰٓؤُلَآءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNdipo akamwomba Mola wake Mlezi: 'Hakika watu hawa ni wakosefu.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأَسْرِ بِعِبَادِى لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMwenyezi Mungu akasema: 'Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱتْرُكِ ٱلْبَحْرَ رَهْوًا إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao ni jeshi litakalozamishwa.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَمْ تَرَكُوا۟ مِن جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMabustani mangapi na chemchemi ngapi waliziacha!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mimea na vyeo vitukufu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَنَعْمَةٍ كَانُوا۟ فِيهَا فَٰكِهِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa neema walizokuwa wakijistareheshea!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَٰهَا قَوْمًا ءَاخَرِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNdio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wengineo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلْأَرْضُ وَمَا كَانُوا۟ مُنظَرِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِىٓ إِسْرَٰٓءِيلَ مِنَ ٱلْعَذَابِ ٱلْمُهِينِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مِن فِرْعَوْنَ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيًا مِّنَ ٱلْمُسْرِفِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterYa Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَقَدِ ٱخْتَرْنَٰهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى ٱلْعَٰلَمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wengineo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَءَاتَيْنَٰهُم مِّنَ ٱلْـَٔايَٰتِ مَا فِيهِ بَلَٰٓؤٌا۟ مُّبِينٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika hawa wanasema:

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنْ هِىَ إِلَّا مَوْتَتُنَا ٱلْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَأْتُوا۟ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمْ صَٰدِقِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَٱلَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ أَهْلَكْنَٰهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا۟ مُجْرِمِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterJe, ni wao bora au watu wa Tubbaa' na waliokuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَا خَلَقْنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَٰعِبِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake kwa mchezo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مَا خَلَقْنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلْحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ يَوْمَ ٱلْفَصْلِ مِيقَٰتُهُمْ أَجْمَعِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika siku ya Uamuzi ni wakati uliowekwa kwa wao wote.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ لَا يُغْنِى مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْـًٔا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIsipokuwa yule mbaye Mwenyezi Mungu atamrehemu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu mno.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika Mti wa Zaqqum

Tazama tafsiri zote za aya hii →

طَعَامُ ٱلْأَثِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNi chakula cha mwenye dhambi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَٱلْمُهْلِ يَغْلِى فِى ٱلْبُطُونِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKama shaba iliyoyeyushwa, hutokota matumboni.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَغَلْىِ ٱلْحَمِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKama kutokota kwa maji ya moto.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

خُذُوهُ فَٱعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلْجَحِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation Center(Itasemwa): 'Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ثُمَّ صُبُّوا۟ فَوْقَ رَأْسِهِۦ مِنْ عَذَابِ ٱلْحَمِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayochemka.'

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ ٱلْعَزِيزُ ٱلْكَرِيمُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterOnja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمْتَرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika haya ndiyo mliyokuwa mkiyatilia shaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى مَقَامٍ أَمِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika wacha Mungu watakuwa katika mahali pa amani.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فِى جَنَّٰتٍ وَعُيُونٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKatika mabustani na chemchemi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَلْبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَقَٰبِلِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWatavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakielekeana.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَذَٰلِكَ وَزَوَّجْنَٰهُم بِحُورٍ عِينٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHivi ndivyo itakavyokuwa, na tutawaoza mahurilaini.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHumo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلْمَوْتَ إِلَّا ٱلْمَوْتَةَ ٱلْأُولَىٰ وَوَقَىٰهُمْ عَذَابَ ٱلْجَحِيمِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHumo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda kutokana na adhabu ya Jahannamu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَضْلًا مِّن رَّبِّكَ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلْفَوْزُ ٱلْعَظِيمُ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَإِنَّمَا يَسَّرْنَٰهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi tumeifanya nyepesi hii Qur-ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱرْتَقِبْ إِنَّهُم مُّرْتَقِبُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNgoja tu, na wao wangoje pia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70