caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Al-Ma'aarij المعارج

Aya 44 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 79

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ سَأَلَ سَآئِلٌۢ بِعَذَابٍ وَاقِعٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMuulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayotokea.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لِّلْكَٰفِرِينَ لَيْسَ لَهُۥ دَافِعٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

مِّنَ ٱللَّهِ ذِى ٱلْمَعَارِجِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

تَعْرُجُ ٱلْمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيْهِ فِى يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُۥ خَمْسِينَ أَلْفَ سَنَةٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMalaika na Roho hupanda kwenda kwake katika siku ambayo kiasi chake ni miaka hamsini elfu!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَٱصْبِرْ صَبْرًا جَمِيلًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi subiri kwa subira njema.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّهُمْ يَرَوْنَهُۥ بَعِيدًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika wao wanaiona iko mbali.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَنَرَىٰهُ قَرِيبًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa Sisi tunaiona iko karibu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلْمُهْلِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku ambayo mbingu zitakapokuwa kama madini iliyoyeyushwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَتَكُونُ ٱلْجِبَالُ كَٱلْعِهْنِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa milima itakuwa kama sufi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَلَا يَسْـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWala jamaa hatamuuliza jamaa yake.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يُبَصَّرُونَهُمْ يَوَدُّ ٱلْمُجْرِمُ لَوْ يَفْتَدِى مِنْ عَذَابِ يَوْمِئِذٍۭ بِبَنِيهِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIjapokuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa mkewe, na nduguye.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِى تُـْٔوِيهِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa jamaa zake waliokuwa wakimkimu,

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَمَن فِى ٱلْأَرْضِ جَمِيعًا ثُمَّ يُنجِيهِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَلَّآ إِنَّهَا لَظَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLa, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,

Tazama tafsiri zote za aya hii →

نَزَّاعَةً لِّلشَّوَىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUnaobambua ngozi ya kichwa!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

تَدْعُوا۟ مَنْ أَدْبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterUtamwita kila aliyegeuza mgongo na akageuka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَجَمَعَ فَأَوْعَىٰٓ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa akakusanya mali, kisha akayahifadhi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ ٱلْإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika mtu ameumbwa na papara.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterInapomgusa shari hupapatika.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَإِذَا مَسَّهُ ٱلْخَيْرُ مَنُوعًا

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa inapomgusa kheri huizuilia.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِلَّا ٱلْمُصَلِّينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIsipokuwa wanaosali.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

ٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ دَآئِمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterAmbao wanadumisha Sala zao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ فِىٓ أَمْوَٰلِهِمْ حَقٌّ مَّعْلُومٌ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ambao katika mali yao iko haki maalumu.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

لِّلسَّآئِلِ وَٱلْمَحْرُومِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwa mwenye kuomba na anayejizuilia kuomba;

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوْمِ ٱلدِّينِ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ambao wanaisadiki Siku ya Malipo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنْ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمْ غَيْرُ مَأْمُونٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuwa na amani nayo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَٰفِظُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ambao wanahifadhi tupu zao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزْوَٰجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَٰنُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterIsipokuwa kwa wake zao, au iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَمَنِ ٱبْتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُو۟لَٰٓئِكَ هُمُ ٱلْعَادُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLakini wanaotaka kinyume cha haya, basi hao ndio wanaoruka mipaka.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ هُمْ لِأَمَٰنَٰتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَٰعُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمْ قَآئِمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,

Tazama tafsiri zote za aya hii →

وَٱلَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa ambao wanazihifadhi Sala zao.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أُو۟لَٰٓئِكَ فِى جَنَّٰتٍ مُّكْرَمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterHao ndio watakaoheshimiwa katika Bustani ya mbinguni.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ قِبَلَكَ مُهْطِعِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterWana nini wale waliokufuru wanakutumbulia macho tu?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

عَنِ ٱلْيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMakundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!

Tazama tafsiri zote za aya hii →

أَيَطْمَعُ كُلُّ ٱمْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُدْخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٍ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Bustani ya mbinguni ya neema?

Tazama tafsiri zote za aya hii →

كَلَّآ إِنَّا خَلَقْنَٰهُم مِّمَّا يَعْلَمُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterLa, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanachokijua.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَلَآ أُقْسِمُ بِرَبِّ ٱلْمَشَٰرِقِ وَٱلْمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ خَيْرًا مِّنْهُمْ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterKuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

فَذَرْهُمْ يَخُوضُوا۟ وَيَلْعَبُوا۟ حَتَّىٰ يُلَٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى يُوعَدُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayoahidiwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

يَوْمَ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ سِرَاعًا كَأَنَّهُمْ إِلَىٰ نُصُبٍ يُوفِضُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterSiku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

خَٰشِعَةً أَبْصَٰرُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ذَٰلِكَ ٱلْيَوْمُ ٱلَّذِى كَانُوا۟ يُوعَدُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterMacho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyokuwa wakiahidiwa.

Tazama tafsiri zote za aya hii →

Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70