Mwanzo › Sura › Sura Al-Burooj
Sura Al-Burooj البروج
Aya 22 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 27
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلْبُرُوجِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ninaapa kwa mbingu yenye nyota kubwa kubwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلْيَوْمِ ٱلْمَوْعُودِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwa Siku iliyoahidiwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَشَاهِدٍ وَمَشْهُودٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na kwa shahidi na kinachoshuhudiwa!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
قُتِلَ أَصْحَٰبُ ٱلْأُخْدُودِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Wameangamizwa watu wa makhandaki.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلْوَقُودِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Yenye moto wenye kuni nyingi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِذْ هُمْ عَلَيْهَا قُعُودٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Walipokuwa wamekaa hapo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَهُمْ عَلَىٰ مَا يَفْعَلُونَ بِٱلْمُؤْمِنِينَ شُهُودٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na wao ni mashahidi wa yale waliyokuwa wakiwafanyia Waumini.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَمَا نَقَمُوا۟ مِنْهُمْ إِلَّآ أَن يُؤْمِنُوا۟ بِٱللَّهِ ٱلْعَزِيزِ ٱلْحَمِيدِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa walikuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ٱلَّذِى لَهُۥ مُلْكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضِ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَىْءٍ شَهِيدٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shahidi wa kila kitu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُوا۟ ٱلْمُؤْمِنِينَ وَٱلْمُؤْمِنَٰتِ ثُمَّ لَمْ يَتُوبُوا۟ فَلَهُمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمْ عَذَابُ ٱلْحَرِيقِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika waliowafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمْ جَنَّٰتٌ تَجْرِى مِن تَحْتِهَا ٱلْأَنْهَٰرُ ذَٰلِكَ ٱلْفَوْزُ ٱلْكَبِيرُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika walioamini na wakatenda mema watapata Bustani za mbinguni zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
إِنَّهُۥ هُوَ يُبْدِئُ وَيُعِيدُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Yeye ndiye anayeanzisha na ndiye anayerejesha tena.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَهُوَ ٱلْغَفُورُ ٱلْوَدُودُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
ذُو ٱلْعَرْشِ ٱلْمَجِيدُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Atendaye ayatakayo.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
هَلْ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلْجُنُودِ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Je! Zimekufikia habari za Majeshi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فِرْعَوْنَ وَثَمُودَ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Ya Firauni na Thamudi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ فِى تَكْذِيبٍ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Lakini waliokufuru wamo katika kukadhibisha.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطٌۢ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazingira.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
بَلْ هُوَ قُرْءَانٌ مَّجِيدٌ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Bali hii ni Qur-ani tukufu.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فِى لَوْحٍ مَّحْفُوظٍۭ
Swahili Translation - Rowad Translation Center Katika Ubao uliohifadhiwa.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
← Sura Al-Inshiqaaq
Sura At-Taariq →
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
→
Matini ya Kiarabu na tafsiri kupitia Tanzil na QuranEnc — kama zilivyo, bila kubadilishwa · Tafsiri ni mali ya watafsiri wake na si Qur'ani yenyewe
Hii ni nyenzo ya utafiti, si chanzo cha fatwa.