Sura Ad-Dhuhaa الضحى
Aya 11 · Makka · mpangilio wa kuteremshwa 11
بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ وَٱلضُّحَىٰ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNinaapa kwa wakati wa kabla ya adhuhuri!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَٱلَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa kwa usiku unapotanda!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterMola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَلْـَٔاخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ ٱلْأُولَىٰ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko uliotangulia.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰٓ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَـَٔاوَىٰ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterKwani hakukukuta yatima, akakupa makazi?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَوَجَدَكَ ضَآلًّا فَهَدَىٰ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa akakukuta umepotea, akakuongoa?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَوَجَدَكَ عَآئِلًا فَأَغْنَىٰ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterAkakukuta mhitaji akakutosheleza?
Tazama tafsiri zote za aya hii →
فَأَمَّا ٱلْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterBasi yatima usimwonee!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَمَّا ٱلسَّآئِلَ فَلَا تَنْهَرْ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa anayeomba au kuuliza usimkaripie!
Tazama tafsiri zote za aya hii →
وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa neema za Mola wako Mlezi zisimulie.
Tazama tafsiri zote za aya hii →
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
→