وَرَفَعْنَا فَوْقَهُمُ ٱلطُّورَ بِمِيثَٰقِهِمْ وَقُلْنَا لَهُمُ ٱدْخُلُوا۟ ٱلْبَابَ سُجَّدًا وَقُلْنَا لَهُمْ لَا تَعْدُوا۟ فِى ٱلسَّبْتِ وَأَخَذْنَا مِنْهُم مِّيثَٰقًا غَلِيظًا
Swahili Translation - Rowad Translation CenterNa tukanyanyua mlima juu yao kwa kufanya agano nao. Na tukawaambia: Ingieni mlangoni kwa kusujudu. Na tukawaambia: Msikiuke mipaka kuhusiana na Siku ya Sabato (Jumamosi). Na tukachukua kwao agano lililo madhubuti.
Swahili Translation - Ali Mohsin Al-BarwaniNa tukanyanyua mlima juu yao kwa kufanya agano nao. Na tukawaambia: Ingilieni mlangoni kwa unyenyekevu. Na tukawaambia: Msiivunje Siku ya Sabato (Jumaa mosi). Na tukachukua kwao ahadi iliyo madhubuti.