caseriqUtafutaji wa maana katika Qur'ani

Sura Al-Maaida, Aya 105

Madina · mpangilio wa kuteremshwa 112 · 5:105

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا ٱهْتَدَيْتُمْ إِلَى ٱللَّهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ

Swahili Translation - Rowad Translation CenterEnyi mlioamini! Kilicho lazima juu yenu ni nafsi zenu. Hatawadhuru mwenye kupotoka ikiwa nyinyi mmeongoka. Ni kwa Mwenyezi Mungu ndiyo marejeo yenu nyote; kisha atawaambia yale mliyokuwa mkiyatenda.
Swahili Translation - Ali Mohsin Al-BarwaniEnyi mlio amini! Kilicho lazima juu yenu ni nafsi zenu. Hawakudhuruni walio potoka ikiwa nyinyi mmeongoka. Ni kwa Mwenyezi Mungu ndio marudio yenu nyote; basi atakwambieni yale mliyo kuwa mkiyatenda.
Unatafuta mada? Jaribu utafutaji wa maana — swali lako hutafutwa katika aya zote 6,236.
Lugha — 70